-
“Vitu Vinavyotamaniwa” Vinaijaza Nyumba ya YehovaMnara wa Mlinzi—2000 | Januari 15
-
-
Lakini siku tatu baada ya kifo chake, Yesu alifufuliwa na Mungu akiwa roho. (1 Petro 3:18) Ndipo angeweza kuingia katika sehemu ya Patakatifu Zaidi Sana ya hekalu la kiroho la Mungu—mbinguni kwenyewe. Na hivyo ndivyo ilivyotokea. Paulo aandika: “Kristo aliingia, si mahali patakatifu [yaelekea akirejezea Patakatifu Zaidi Sana] palipofanywa kwa mikono, ambapo ni nakala ya uhalisi, bali mbinguni kwenyewe, ili sasa aonekane mbele ya uso wa Mungu kwa ajili yetu.”—Waebrania 9:24.
10. Yesu alifanya nini aliporudi mbinguni?
10 Akiwa mbinguni, Yesu ‘alinyunyiza damu’ ya dhabihu yake kwa kutoa thamani ya damu yake ya fidia yenye uhai mbele za Yehova. Lakini, Yesu alifanya mengi hata zaidi. Muda mfupi kabla ya kifo chake, aliwaambia wafuasi wake: “Nashika njia yangu kwenda kuwatayarishia nyinyi mahali. Pia, nikishika njia yangu kwenda na kuwatayarishia nyinyi mahali, mimi ninakuja tena na hakika nitawapokea nyinyi nyumbani kwangu mwenyewe, ili mahali nilipo nyinyi pia mpate kuwa.” (Yohana 14:2, 3) Hivyo, kwa kuingia katika Patakatifu Zaidi Sana, au mbinguni, Yesu aliwafungulia njia wengine waingie pia. (Waebrania 6:19, 20) Watu hawa, ambao wangekuwa 144,000, wangetumikia wakiwa makuhani wa cheo cha chini katika mpango wa Mungu wa hekalu la kiroho. (Ufunuo 7:4; 14:1; 20:6) Kama vile tu kuhani wa cheo cha juu wa Israeli alivyopeleka kwanza damu ya fahali katika Patakatifu Zaidi Sana ili kufunika dhambi za makuhani, thamani ya damu ya Yesu iliyomwagika ilitumiwa kwanza kwa makuhani hao 144,000 wa cheo cha chini.b
-
-
“Vitu Vinavyotamaniwa” Vinaijaza Nyumba ya YehovaMnara wa Mlinzi—2000 | Januari 15
-
-
b Tofauti na kuhani wa cheo cha juu wa Israeli, Yesu hakuwa na dhambi za kufunika. Lakini, makuhani wenzake walikuwa wenye dhambi kwa sababu walinunuliwa kutoka miongoni mwa wanadamu wenye dhambi.—Ufunuo 5:9, 10.
-