Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Alinifundisha Kufanya Mapenzi Yake
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
    • KAZI YA MZUNGUKO NA GILEADI

      Baada ya kuhubiri katika mgawo huo kwa miezi minane hivi, nilipokea mwaliko kutoka kwenye Ofisi ya Tawi ya Australia, mwaliko wa kuwa mwangalizi wa mzunguko. Mwaliko huo ulinishtua kwa sababu nilikuwa na umri wa miaka 20 tu. Baada ya kuzoezwa kwa majuma kadhaa, nilianza kutembelea makutaniko kwa ukawaida ili kuyatia moyo. Watu wenye umri mkubwa kuliko mimi, yaani, karibu kila mtu, hawakunidharau kwa sababu nilikuwa kijana lakini waliheshimu kazi niliyokuwa nikifanya.

      Kila kutaniko nililotembelea lilitofautiana kama nini na lile lingine! Juma moja nilisafiri kwa basi, juma lingine kwa gari-moshi la umeme, kisha nilisafiri kwa gari au nilibebwa kwenye pikipiki, huku nikiwa nimebeba sanduku na mkoba wa mahubiri. Kukaa na Mashahidi wenzangu kuliniletea shangwe ya kweli. Mtumishi mmoja wa kampuni alikuwa na hamu ya kukaa pamoja nami hata ingawa nyumba yake haikuwa imemalizika kujengwa. Juma hilo nililala ndani ya beseni kubwa la kuogea, lakini sote tulifurahia kama nini mambo ya kiroho juma hilo!

  • Yehova Alinifundisha Kufanya Mapenzi Yake
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
    • [Blabu katika ukurasa wa 19]

      Juma moja nilisafiri kwa basi, juma lingine kwa gari-moshi la umeme, kisha nilisafiri kwa gari au nilibebwa kwenye pikipiki, huku nikiwa nimebeba sanduku na mkoba wa mahubiri

  • Yehova Alinifundisha Kufanya Mapenzi Yake
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
    • [Picha katika ukurasa wa 18]

      Kushoto: Nikiwa katika kazi ya mzunguko huko Australia

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki