Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mahali Ngamia na Farasi Hurandaranda
    Amkeni!—2001 | Aprili 8
    • Hata hivyo wanyama wengi zaidi katika eneo hilo ni punda-mwitu mwenye umbo linaloshabihi farasi-mwitu. Imekuwa lazima kuwapunguza wanyama hao wanaozaana sana kuliko farasi-mwitu na kuzagaa kwenye eneo kubwa kuliko ngamia.

      Mbinu ya Yudasi

      Punda, kama ilivyotukia na farasi, waliingizwa Australia mapema miaka ya 1700 kwa kusudi la kukokota mizigo au kuvuta plau, na walizoea upesi mazingira mapya. Baada ya punda wengi kuachiliwa huru katika miaka ya 1920, idadi yao iliongezeka na kuwa mara 30 ya idadi ya awali ya makundi ya punda-mwitu.

      Kama ngamia, punda ameumbwa kuishi jangwani, ana uwezo wa kuzuia jasho lisimtoke anapoishiwa na maji na anaweza kustahimili kupoteza maji yanayolingana na asilimia 30 ya uzani wake. (Wanyama wengine hufa wanapopoteza maji yanayolingana na asilimia 12 hadi 15 ya uzani wao.) Wao hufurahia kula majani mororo lakini wanaweza pia kula majani makavu yasiyoliwa na ng’ombe. Kufikia miaka ya 1970, punda zaidi ya 750,000 walizagaa katika nusu ya bara hilo la Australia. Idadi hiyo yenye kuongezeka ilisababisha matatizo ya mazingira na kutatiza ufugaji wa ng’ombe hivyo ikalazimu hatua fulani ichukuliwe.

      Jitihada ya kuwapunguza katika miaka ya 1978 hadi 1993 ilisababisha punda 500,000 kuuawa huko kaskazini-magharibi mwa Australia pekee. Leo, punda 300 wamewekwa mwilini mwao kifaa cha radio katika mpango unaojulikana kama mbinu ya Yudasi. Baada ya kuachwa huru kujiunga na wenzao, kifaa hicho cha radio kilicho mwilini mwa punda huwaongoza watu walio kwenye helikopta hadi mahali walipo punda wengi na punda hao hupunguzwa kwa kuuawa bila ukatili. Baadaye punda mwenye kifaa cha radio mwilini hujiunga na kundi jingine la punda na hivyo kuwaongoza waangamizaji kwa kundi hilo pia.

      “Hilo ni tatizo la kudumu,” ofisa mmoja wa ulinzi wa mifugo kutoka eneo la Magharibi mwa Australia aliliambia Amkeni! Alionya hivi: “Kundi la punda wachache wenye kuzaana likisalia, baada ya muda mfupi kutakuwa na idadi kubwa ya punda kama ile ya miaka ya 1970. Watu wengi hushangaa kuona wanyama hao wakiuawa na mizoga kuachwa palepale. Hawafahamu kwamba maeneo hayo hayafikiki. Maeneo hayo hayana barabara na sehemu nyingi hufikiwa tu kwa helikopta. Ni matendo ya binadamu yaliyosababisha tatizo hilo na hivyo tunajaribu kuangamiza hao punda kwa namna isiyo na ukatili tuwezavyo.”

  • Mahali Ngamia na Farasi Hurandaranda
    Amkeni!—2001 | Aprili 8
    • [Picha katika ukurasa wa 18]

      Punda awekwa kifaa cha radio katika ile mbinu ya Yudasi

      [Hisani]

      Agriculture Western Australia

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki