-
Ole wa Pili—Majeshi ya Wapanda-FarasiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Kwa maana mamlaka yao imo katika vinywa vyao na katika mikia yao; kwa maana mikia yao ni kama manyoka na ina vichwa, na kwa hivyo wao hufanya dhara.” (Ufunuo 9:19, NW) Yehova ameweka rasmi wahudumu wake walio wakfu na kubatizwa kwa ajili ya utumishi huu. Yeye amewafundisha jinsi ya ‘kuhubiri neno’ kupitia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na mikutano mingine ya kundi na mashule, hivi kwamba wanapata uwezo wa kusema kwa mamlaka kwa “ulimi wa waliofundishwa.” Yeye ameweka maneno yake katika vinywa vyao na akawatuma watoke kwenda kujulisha hukumu zake “peupe na kutoka nyumba kwa nyumba.” (2 Timotheo 4:2; Isaya 50:4; 61:2; Yeremia 1:9, 10; Matendo 20:20, NW)
-
-
Ole wa Pili—Majeshi ya Wapanda-FarasiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
17. Je! Mashahidi wa Yehova wana sehemu yoyote katika shambulio la majeshi ya wapanda-farasi katika yale mabara ambako fasihi haziwezi kuenezwa kwa sababu kazi ni marufuku? Fafanua.
17 Washiriki wa sehemu yenye bidii zaidi sana ya haya majeshi ya wapanda-farasi ni ndugu walio katika mabara ambako kazi ya Mashahidi wa Yehova ni marufuku. Kama kondoo katikati ya mbwa-mwitu, hawa hawana budi kuwa “wenye tahadhari kama nyoka na hata hivyo bila hatia kama njiwa.” Kwa kutii Yehova wao ‘hawawezi kuacha kusema vitu ambavyo wameona na kusikia.’ (Mathayo 10:16; Matendo 4:19, 20; 5:28, 29, 32, NW) Kwa kuwa wana vifaa vichache vilivyochapwa vya kugawa peupe au hawana kabisa, je! ni lazima sisi tukate kauli kwamba wao hawana hisa katika shambulio la majeshi ya wapanda-farasi? Sivyo hata kidogo! Wao wana vinywa vyao na mamlaka kutoka kwa Yehova kuvitumia kusema ukweli wa Biblia. Wao wanafanya hivyo, vivi hivi na kwa usadikishi, wakianzisha mafunzo katika Biblia na ‘wakileta wengi kwenye uadilifu.’ (Danieli 12:3, NW) Ingawa huenda wao wasichome kwa uchungu kwa mikia yao katika maana ya kuacha nyuma fasihi zenye kupiga sana, moto, moshi, na salfa vya mfano hutoka katika vinywa vyao wanapotoa ushuhuda kwa busara na kwa uangalifu kuhusu siku ya utetezi ya Yehova inayokaribia.
-