-
“Kristo Ni Nguvu ya Mungu”Mkaribie Yehova
-
-
Baadaye, Yehova alimpa Mwana huyo mamlaka na nguvu nyingi sana. Alimpa kazi ya kutimiza makusudi Yake ya uumbaji. Biblia yasema hivi kumhusu Mwana huyo: “Vitu vyote vilikuja kuwako kupitia yeye, na bila yeye hata kitu kimoja hakikuja kuwako.”—Yohana 1:3.
5 Hatuwezi kufahamu kikamili uzito wa kazi hiyo.
-
-
“Kristo Ni Nguvu ya Mungu”Mkaribie Yehova
-
-
6. Baada ya kufa na kufufuliwa, Yesu alipewa nguvu na mamlaka gani?
6 Je, Mwana huyo mzaliwa-pekee angeweza kupewa nguvu na mamlaka zaidi? Yesu alisema hivi baada ya kufa na kufufuliwa: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na juu ya dunia.” (Mathayo 28:18) Naam, Yesu alikuwa amepewa uwezo na haki ya kutawala ulimwengu mzima. Akiwa “Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana,” amepewa mamlaka ya kufanya “serikali yote na mamlaka yote na nguvu”—zinazoonekana na zile zisizoonekana—ambazo zinampinga Baba yake “kuwa si kitu.” (Ufunuo 19:16; 1 Wakorintho 15:24-26) ‘Vitu vyote vilitiishwa chini ya’ Yesu, ila Yehova Mungu mwenyewe.—Waebrania 2:8; 1 Wakorintho 15:27.
-