-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kwa mfano, huko Hispania, Sandra mwenye umri wa miaka 11 na kaka yake, Alejandro, mwenye umri wa miaka 7, walitaka kuongeza utumishi wao. Walichochewa na bidii ya ndugu wa kutaniko lao na mfano mzuri wa wazazi wao, na wakatamani kuwa mapainia wasaidizi. Wangefanyaje hivyo ilhali hawajabatizwa? Wote wawili walipanga ratiba ya kutumia wakati sawa na wa wazazi wao katika utumishi, na kujitayarisha kwa kuwa na vipindi vya mazoezi wakati wa jioni ya Ibada ya Familia. Wazazi wao walifikiri kwamba kadiri mwezi ulivyosonga, watoto hao wangechoka. Lakini watoto hao hawakuyumba-yumba. Kufikia ApriliĀ 30, wote katika familia hiyo walikuwa wametimiza mradi wao wa saa 30 isipokuwa Alejandro, ambaye bado alihitaji saa tatu. Hivyo, akaenda kuhubiri na baba yake ili atimize lengo lake la mwezi huo. Walifurahi kama nini kuwa na wakati mzuri na kufanya mengi wakiwa familia iliyoungana!
-
-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 11]
Alejandro na baba yake katika siku ya mwisho ya mwezi katika eneo la Sant Celoni, Barcelona, Hispania
-