Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’
    Huduma ya Ufalme—2002 | Machi
    • 4 Twaweza kuonyeshaje kwamba sisi ni “matajiri katika kazi zilizo bora” wakati wa majira haya ya Ukumbusho? Kwa kuendelea kushiriki katika kazi ya kuhubiri habari njema kwa uchangamfu, kuwa “wenye bidii kwa kazi zilizo bora.” (Tito 2:14; Mt. 24:14) Ikiwa hukuweza kufanya upainia msaidizi mwezi wa Machi, je, waweza kufanya hivyo mwezi wa Aprili/au Mei? Ikiwa unafanya upainia mwezi huu, je, waweza kuendelea?

      5 Watu wengine wanaofanya kazi ya kimwili wameona kwamba wanaweza kutumia muda wa saa moja au zaidi katika utumishi wanapokwenda kazini, kwa kuwahubiria watu barabarani au kwa kuwahubiria wale ambao huanza biashara zao asubuhi na mapema. Wengine wamepanga kuhubiri saa za chakula cha mchana. Wengine wameweza kuongoza funzo la Biblia na mfanyakazi mwenzao katika kipindi hicho. Akina dada wengi ambao hawajaajiriwa wameweza kutenga wakati kwa ajili ya huduma ya shambani watoto wao wanapokuwa shuleni. Kwa kuamka mapema kidogo siku fulani ili kufanya kazi zao za nyumbani, wamepata nafasi ya kuhubiri na kufundisha wakati wa mchana.—Efe. 5:15, 16.

  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’
    Huduma ya Ufalme—2002 | Machi
    • Wengi ambao wamefanya upainia-msaidizi kwa mwezi mmoja au zaidi wameona kwamba utumishi wao wa shambani umeongezeka katika miezi inayofuata. Walikutana na watu wenye kupendezwa na wakawarudia. Hiyo iliwachochea wajitahidi kwenda katika utumishi wa shambani mara nyingi ili kuwatembelea tena watu hao wenye kupendezwa. Wengine walianzisha mafunzo ya Biblia, na hilo liliwasaidia kushiriki zaidi katika huduma.

      13 Na wengine wamepata shangwe nyingi kwa kufanya mengi zaidi katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi hivi kwamba walichochewa kuchunguza mambo wanayopaswa kutanguliza. Tokeo ni kwamba, wengine waliweza kupunguza muda wanaotumia katika kazi ya kimwili na kuendelea kuwa mapainia-wasaidizi. Wengine wameanza utumishi wa painia wa kawaida. Hawakutumaini vitu vya ulimwengu huu, bali walimtumaini Mungu kabisa. Waliona kwamba kuwa “wakarimu, tayari kushiriki,” kuliwaletea baraka tele kutoka kwa Yehova na kuliimarisha tumaini lao la kufurahia “uhai ulio halisi.” (1 Tim. 6:18, 19) Bila shaka, wengi wafanyapo upainia, kutaniko zima hunufaika. Mapainia hupenda kuongea juu ya mambo yaliyoonwa na kualika wengine washiriki katika huduma pamoja nao, na hiyo huchochea hali nzuri ya kiroho katika kutaniko.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki