Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ni “Mfunuaji wa Siri”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Juni 15
    • KICHWA CHA TATU—BABILONI

      9, 10. (a) Yehova aliwaruhusu Wababiloni wafanye nini? (b) Ili unabii utimie, ilikuwa lazima mambo gani yatukie?

      9 Kichwa cha tatu cha mnyama-mwitu ambaye Yohana aliona kinafananisha ufalme wenye mji mkuu ulioitwa Babiloni. Yehova aliwaruhusu Wababiloni walishinde jiji la Yerusalemu na kuwapeleka watu wake utekwani. Hata hivyo, kabla ya kuruhusu Waisraeli waaibishwe kwa njia hiyo, Yehova aliwaonya watu hao walioasi kwamba msiba huo ungewapata. (2 Fal. 20:16-18) Alitabiri kwamba ukoo wa wafalme wa kibinadamu ambao ilisemekana kwamba wanaketi juu ya “kiti cha ufalme cha Yehova” huko Yerusalemu ungeondolewa. (1 Nya. 29:23) Hata hivyo, Yehova pia aliahidi kwamba mzao wa Mfalme Daudi, mzao ambaye alikuwa na “haki ya kisheria,” angekuja na kuchukua mamlaka hayo.—Eze. 21:25-27.

      10 Unabii mwingine ulionyesha kwamba bado Wayahudi wangekuwa wakiabudu kwenye hekalu la Yerusalemu wakati wa kuja kwa Masihi au Mtiwa-Mafuta aliyeahidiwa. (Dan. 9:24-27) Unabii fulani ulioandikwa mapema kabla ya Waisraeli kupelekwa utekwani Babiloni, ulisema kwamba huyo Masihi angezaliwa Bethlehemu. (Mika 5:2) Ili unabii huo mbalimbali utimie, Wayahudi wangehitaji kuwekwa huru kutoka utekwani, warudi katika nchi yao, na kujenga upya hekalu. Lakini sheria za Wababiloni hazikuruhusu mateka waachiliwe huru. Tatizo hilo lingetatuliwaje? Yehova aliwafunulia manabii wake jibu la swali hilo.—Amo. 3:7.

      11. Ni mifano gani mbalimbali inayotumiwa kufananisha Milki ya Babiloni? (Tazama maelezo ya chini.)

      11 Nabii Danieli alikuwa miongoni mwa mateka waliopelekwa Babiloni. (Dan. 1:1-6) Yehova alimtumia kufunua jinsi ambavyo falme zingefuatana baada ya serikali hiyo kuu ya ulimwengu kuanguka. Yehova alifunua siri hizo akitumia mifano mbalimbali. Kwa mfano, alimletea Mfalme Nebukadneza wa Babiloni ndoto kuhusu sanamu kubwa sana ambayo ilitengenezwa kwa madini ya aina mbalimbali. (Soma Danieli 2:1, 19, 31-38.) Kupitia Danieli, Yehova alifunua kwamba kichwa cha dhahabu cha sanamu hiyo kilifananisha Milki ya Babiloni.b

  • Yehova Ni “Mfunuaji wa Siri”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Juni 15
    • b Babiloni inafananishwa na kichwa cha ile sanamu katika kitabu cha Danieli na pia kichwa cha tatu cha yule mnyama-mwitu wa kitabu cha Ufunuo. Tazama chati kwenye ukurasa wa 12-13.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki