Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuirudia Ibada ya Yehova
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 1. Miungu miwili kati ya miungu mikuu ya Babiloni inaitwaje, na ni nini kinachotabiriwa kuihusu?

      ISRAELI watakapopelekwa uhamishoni Babiloni, watazungukwa na ibada ya uwongo. Wakati wa Isaya, watu wa Yehova bado wamo katika nchi yao wenyewe, na wana hekalu na ukuhani. Hata hivyo, wengi katika taifa lililo wakfu wamejiacha washindwe na ibada ya sanamu. Basi ni muhimu kuwatayarisha mapema wasiihofu mno miungu ya uwongo ya Babiloni wala kushawishika kuitumikia. Hivyo basi, Isaya anatoa unabii kuhusu miwili kati ya miungu mikuu ya Babiloni, akisema hivi: “Beli anaanguka chini, Nebo anainama; sanamu zao ziko juu ya wanyama, na juu ya ng’ombe; vitu vile mlivyokuwa mkivichukua huku na huku vimekuwa mzigo, mzigo wa kumlemea mnyama aliyechoka.” (Isaya 46:1) Beli ndiye mungu-sanamu aliye mkuu miongoni mwa Wakaldayo. Naye Nebo anaheshimiwa sana kuwa mungu wa hekima na masomo. Watu wengi wanaiheshimu miungu hiyo miwili, na hiyo inaonekana wazi kwa kuwa majina ya miungu hiyo yanahusishwa katika majina kadhaa ya Wababiloni binafsi—Belshaza, Nabopolasa, Nebukadreza, na Nebuzaradani, kutaja machache tu.

      2. Kutojiweza kwa miungu ya Babiloni kunatiliwaje mkazo?

      2 Isaya anasema kwamba Beli ‘ameanguka chini,’ na Nebo “anainama.” Miungu hiyo ya uwongo itabwagwa chini. Haitaweza kuwasaidia waabudu wake Yehova aletapo hukumu zake juu ya Babiloni. Hata haitaweza kujiokoa yenyewe, ng’o! Beli na Nebo hawatabebwa tena katika mahali pa heshima wakati wa maandamano, kama yale ya kuadhimisha sherehe za Siku ya Mwaka Mpya wa Babiloni. Bali, waabudu wao watawakokota kama mizigo ya kawaida. Badala ya kusifiwa na kutukuzwa, miungu hiyo itazomewa na kudharauliwa.

      3. (a) Wababiloni watagutushwa na nini? (b) Kilichoipata miungu ya Babiloni kinaweza kuwa na somo gani leo?

      3 He, acha Wababiloni wagutuke wanapotambua kwamba kumbe sanamu zao vipenzi ni mizigo tu inayobebwa na wanyama wachovu!

  • Kuirudia Ibada ya Yehova
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • [Picha katika ukurasa wa 94]

      Miungu ya Babiloni inashindwa kumlinda na uharibifu

  • Kuirudia Ibada ya Yehova
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 4. Miungu ya Babiloni ‘inajiinamisha’ na ‘kuinama’ katika maana gani?

      4 Unabii unazidi kukazia kushindwa kabisa kwa miungu ya Babiloni, unaposema hivi: “Wanajiinamisha, wanainama pamoja; hawakuweza kuutua mzigo [“kuupatia mzigo njia ya kuokoka,” “NW”], bali wao wenyewe wamekwenda kufungwa.” (Isaya 46:2) Inaonekana miungu ya Babiloni ‘inajiinamisha’ na ‘kuinama’ kana kwamba imejeruhiwa vitani au ikawa vizee vinyonge. Hata haiwezi kuupunguza mzigo wa wanyama duni wanaoibeba, wala kuwapa njia ya kuokokea. Mambo yakiwa hivyo, je, watu wa agano la Yehova wanapaswa kweli kuiheshimu miungu hiyo kwa vyovyote, hata ingawa wao ni mateka Babiloni? La!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki