-
‘Nafsi Zilizochinjwa’ ZathawabishwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
7. Ni nani hasa mwenye hatia ya ‘umwagaji-damu ya watakatifu’?
7 Kama vile katika nyakati za Biblia, ndivyo na leo, wengi wa wale watu mmoja mmoja walioua mashahidi wa Mungu huenda wamekufa kitambo. Lakini tengenezo lililosababisha ufia-imani wao lingali hai sana na ni lenye hatia ya damu. Ni tengenezo la Shetani la kidunia, mbegu yake ya kidunia. Sehemu yenye kutokeza katika hiyo ni Babuloni Mkubwa, ile milki ya ulimwengu ya dini bandia.a Yeye anaelezwa kuwa ‘amelewa kwa damu ya watakatifu na kwa damu ya mashahidi wa Yesu.’ Ndiyo, “katika yeye ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu na ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” (Ufunuo 17:5, 6; 18:24; Waefeso 4:11; 1 Wakorintho 12:28, NW)
-
-
‘Nafsi Zilizochinjwa’ ZathawabishwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
9. (a) Ni kipeo gani cha udanganyifu alichotokeza Shetani kufikia karne ya nne W.K., nacho ni sehemu kuu ya nini? (b) Baadhi ya watawala wa Jumuiya ya Wakristo waliwatendeaje Mashahidi wa Yehova wakati wa Vita ya Ulimwengu 1 na 2?
9 Kufikia karne ya nne W.K., yule nyoka wa zamani, Shetani Ibilisi, alikuwa ametokeza kipeo cha udanganyifu wake, ile dini yenye uasi-imani ya Jumuiya ya Wakristo—mfumo wa Kibabuloni uliofichwa chini ya kibandiko cha “Ukristo.” Ndiyo sehemu iliyo kuu ya mbegu ya yule Nyoka na imesitawi ikawa umati wa farakano zenye kuhitilafiana. Kama Yuda ya kale isiyo na imani, Jumuiya ya Wakristo inabeba hatia nzito ya damu, ikiwa imekwisha kujihusisha sana katika pande zote mbili za Vita ya Ulimwengu 1 na 2. Wengine wa watawala wa kisiasa wa Jumuiya ya Wakristo hata walitumia vita hivyo kuwa kisababu cha kuchinja watumishi wa Mungu.
-