-
“Saa Ya Hukumu” ImefikaEndeleeni Kukesha!
-
-
Sasa uharibifu wake wa mwisho umekaribia. Kwa sababu hiyo, Biblia inawahimiza watu wote hivi: “Tokeni kwake [Babiloni Mkubwa] . . . ikiwa hamtaki kushiriki pamoja naye dhambi zake, na ikiwa hamtaki kupokea sehemu ya mapigo yake. Kwa maana dhambi zake zimekusanyika pamoja mpaka mbinguni, naye Mungu amekumbuka matendo yake yasiyo ya haki.”—Ufunuo 18:4, 5.
-
-
“Saa Ya Hukumu” ImefikaEndeleeni Kukesha!
-
-
Unapaswa kuchukua hatua gani? Jiulize: ‘Je, bado mimi ni mfuasi wa dini ambayo imechafuliwa na mafundisho na mazoea yanayoifanya kuwa sehemu ya Babiloni Mkubwa?’ Hata kama wewe si mfuasi wa dini kama hiyo, huenda ukajiuliza: ‘Je, nimeruhusu roho yake iniathiri?’ Roho gani? Roho ya kukubali maadili mapotovu, kupenda mali na raha badala ya kumpenda Mungu, au kupuuza kimakusudi Neno la Yehova (hata katika mambo yanayoonekana kuwa madogo). Fikiria kwa uzito jibu lako.
Ili tupate kibali cha Yehova ni muhimu tuonyeshe kwa matendo na kutoka moyoni kwamba kwa kweli sisi si sehemu ya Babiloni Mkubwa. Huu si wakati wa kukawia-kawia. Ikituonya kwamba mwisho utakuja ghafula, Biblia inasema: ‘Babiloni lile jiji kubwa litatupwa chini kwa mtupo wa kasi sana, naye hatapatikana tena.’—Ufunuo 18:21.
-