-
Yehova Hakutuacha KamweMnara wa Mlinzi—1996 | Januari 1
-
-
Katika Aprili 1939, kabla tu ya mwanzo wa Vita ya Ulimwengu 2, vikosi vya Ufashisti vya Kiitalia vilishambulia Albania. Upesi baada ya hilo kazi ya Mashahidi wa Yehova ilipigwa marufuku, lakini kikundi chetu kidogo cha wapiga-mbiu wa Ufalme karibu 50 kiliendelea kuhubiri. Vitabu na vijitabu vyetu vipatavyo 15,000 vilitwaliwa na kuharibiwa wakati wa Vita ya Ulimwengu 2.
-
-
Yehova Hakutuacha KamweMnara wa Mlinzi—1996 | Januari 1
-
-
Hata ingawa kazi yetu ilikuwa imepigwa marufuku na Vita ya Ulimwengu 2 iliendelea katika nchi zilizotuzunguka, tuliendelea kufanya kile ambacho tungeweza ili kutimiza utume wetu wa kuhubiri ujumbe wa Ufalme. (Mathayo 24:14) Katika 1944 jumla ya Mashahidi 15 walikuwa gerezani. Hata hivyo, katika nyakati hizo ngumu, hatukuhisi kamwe kuwa tumeachwa na Yehova.
-