-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
Dalili Nyingine za Mabadiliko
Hotuba ya rais na mkutano aliofanya na waandishi wa habari Aprili 24, 1990, ulionyesha kwamba maoni ya serikali kuwahusu Mashahidi wa Yehova yalikuwa yamebadilika sana. Rais aliwahakikishia waandishi wa habari nchini na wa kigeni kwamba serikali inatetea uhuru wa msingi, kutia ndani uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kidini. Hivyo ndugu walitumia nafasi hiyo kuhubiri na kukutana waziwazi zaidi. Wale waliokuwa gerezani waliachiliwa.
-
-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
Uhuru Tena
Amri ya rais ya mwaka wa 1986 ilipiga marufuku utendaji wote wa Mashahidi wa Yehova, na ikavunja shirika lao la kisheria nchini humo. Hata hivyo, Januari 8, 1993, Mahakama Kuu ya Sheria ya Zaire (Kongo) ilitoa uamuzi wa Kesi Kati ya Mashahidi wa Yehova na Jamhuri ya Zaire. Mahakama hiyo iliamua kwamba agizo la rais halikuwa la haki, na hivyo likafutiliwa mbali. Ndugu walikuwa na furaha iliyoje!
Uamuzi wa Mahakama Kuu ulizusha ubishi mkali kwa sababu mahakama hiyo ilifuata katiba mpya ya mabadiliko, ambayo haikukubaliwa na rais na wale waliomuunga mkono. Baadhi ya watu waliona uamuzi huo kuwa kielelezo cha kutumiwa wakati ujao na mahakama. Mashahidi hawakushiriki ubishi huo, lakini ushahidi mkubwa sana ulitolewa kwa utukufu wa jina la Yehova! Magazeti mengi yalizungumzia kesi hiyo muhimu. Kisha Idara ya Sheria iliwajulisha magavana wa majimbo mbalimbali kwamba Mashahidi wa Yehova waliruhusiwa kisheria kuendelea na utendaji wao wa kidini. Ulikuwa ushindi ulioje kwa watu wa Yehova na kwa ibada ya kweli!
-