-
Mwanavita-Mfalme Asherehekea Ushindi Kwenye Har–MagedoniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Na hayawani-mwitu akabambwa, na pamoja na yeye nabii bandia ambaye alifanya mbele yake ishara ambazo kwa hizo yeye aliongoza vibaya wale ambao walipokea alama ya hayawani-mwitu na wale ambao hutoa ibada kwa mfano wake. Wakiwa wangali hai, wao wawili walivurumishwa ndani ya ziwa lenye moto ambalo huwaka salfa.
-
-
Mwanavita-Mfalme Asherehekea Ushindi Kwenye Har–MagedoniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
24. (a) Ni hukumu gani inayotekelezwa juu ya hayawani-mwitu na juu ya nabii bandia, na ni katika maana gani wao “wakiwa wangali hai”? (b) Kwa nini “ziwa la moto” lazima liwe la kitamathali?
24 Hayawani-mwitu mwenye vichwa saba na pembe kumi kutoka katika bahari, akiwakilisha tengenezo la kisiasa la Shetani, anatumbukizwa ndani ya usahaulifu kabisa, na pamoja na yeye aenda nabii bandia, serikali ya saba ya ulimwengu. (Ufunuo 13:1, 11-13; 16:13) Wakiwa wangali “hai,” au wangali wanatenda katika umoja wao wa kuwapinga watu wa Mungu duniani, wao wanatupwa ndani ya “ziwa la moto.” Je! hili ni ziwa halisi la moto? La, kama vile hayawani-mwitu na nabii bandia wasivyokuwa wanyama halisi. Badala ya hivyo, ni ufananisho wa uharibifu kamili wa mwisho kabisa, mahali ambako hakuna kurudi.
-