Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sababu Nzuri ya Kumwamini Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Desemba 1
    • Sababu Nzuri ya Kumwamini Mungu

      KITABU cha Kikorea kinachoitwa 31 Reasons Why Young People Leave the Church kinasisitiza kwamba wengi wanaacha kwenda kanisani kwa sababu hawapati majibu yenye kuridhisha kwa maswali yao. Kwa mfano, wanauliza, ‘Kwa nini watu wanaomwamini Mungu wanateseka?’ na ‘Kwa nini ni lazima tuamini kila jambo linalofundishwa katika makanisa na huku mengi ya mafundisho hayo yanatatanisha na kupingana?’

      Kwa sababu wamekatishwa tamaa na majibu wanayopewa na makasisi wao, wengi huamua kwamba hakuna jibu katika Biblia. Kasisi anapotoa maelezo yanayotegemea maoni yake tu, mara nyingi matokeo huwa kutomwelewa, hata kumkataa, Mungu na Biblia.

      Hayo ndiyo yaliyompata Abel, aliyelelewa katika Kanisa la Kilutheri nchini Afrika Kusini. Anakumbuka hivi: “Kanisa hufundisha kwamba kila mtu anayekufa ‘huchukuliwa’ na Mungu. Lakini sikuelewa kwa nini Mungu mwenye upendo ‘angewachukua’ wazazi na kuwaacha watoto peke yao. Katika maeneo ya vijijini Afrika, nilikokulia, hatukumchinja kuku akiwa na vifaranga wachanga. Tukitambua kwamba ng’ombe alikuwa na mimba, hatukumchinja mpaka alipozaa na kumaliza kunyonyesha. Sikuweza kuelewa kwa nini Mungu mwenye upendo hakuwajali wanadamu kwa njia hiyohiyo.”

      Aram, kutoka Kanada, alikuwa na shaka hizohizo. Yeye anasema, “baba yangu alikufa nilipokuwa na umri wa miaka 13. Katika mazishi, kasisi mashuhuri alisema kwamba Mungu alitaka baba yangu afe ili amkaribie mbinguni. Alisema, ‘Mungu huwachukua watu wazuri kwa sababu anawapenda watu waadilifu.’ Sikuelewa kwa nini Mungu awe mchoyo kiasi hicho.”

  • Sababu Nzuri ya Kumwamini Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Desemba 1
    • [Sanduku katika ukurasa wa 6]

      Maswali Magumu Yaliyohitaji Majibu

      “Nilipokuwa nikizoezwa hospitalini nikiwa mwanafunzi wa udaktari, niliona watu wema wakiugua kwa maumivu kwa sababu ya magonjwa na misiba. Ikiwa kuna Mungu, kwa nini mambo hayo yanatendeka? Je, dini ni njia tu ya kupata amani ya akili?”—Aliyekuwa Mpresibiteri nchini Korea.

      “Mara nyingi nilijiuliza ikiwa baba yangu, aliyekuwa mlevi, alienda motoni au mbinguni. Niliwaogopa sana wafu na moto wa mateso. Sikuelewa kwa nini Mungu mwenye upendo angeweza kumpeleka mtu ateseke milele motoni.”—Aliyekuwa Mkatoliki nchini Brazili.

      “Kuna tazamio gani la wakati ujao kwa ajili ya dunia na wanadamu? Wanadamu watawezaje kuishi milele? Wanadamu watapataje amani ya kweli?”—Aliyekuwa Mkatoliki nchini Ujerumani.

      “Sikuelewa fundisho la kuzaliwa upya katika umbo jingine. Wanyama hawaabudu, kwa hiyo ikiwa unazaliwa upya katika umbo jingine ukiwa mnyama ili kulipia dhambi zako, utarekebishaje mambo na kufanya maendeleo ukiwa mnyama?”—Aliyekuwa Mhindu nchini Afrika Kusini.

      “Nililelewa katika familia ya Wakonfyushasi, nami nilishiriki katika sherehe za kuwatuliza mababu Wetu waliokufa. Nilipokuwa nikishiriki katika kupanga meza ya dhabihu na kusujudu, nilijiuliza ikiwa hao mababu waliokufa walikuja kula chakula hicho na kuona tukiwasujudia.”—Aliyekuwa Mkonfyushasi nchini Korea.

      Watu hao wote walipata majibu kwa maswali yao walipojifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki