-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Sura ya 10
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
MASHAHIDI WA YEHOVA hawajakusudia kuanzisha mafundisho mapya, njia mpya ya ibada, dini mpya. Badala ya hivyo, historia yao ya kisasa huonyesha jitihada ya kudhamiria ya kufundisha yale yanayopatikana katika Biblia, Neno la Mungu lililopuliziwa. Wao huelekeza kwalo likiwa msingi wa imani zao zote na njia yao ya maisha. Badala ya kusitawisha imani ambazo huonyesha mielekeo yenye kuendekeza ya ulimwengu wa kisasa, wao huendelea kujitahidi kujipatanisha kwa ukaribu zaidi na mafundisho na mazoea ya Kibiblia ya Ukristo wa karne ya kwanza.
-
-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Je, wao waliamini kwamba walikuwa na majibu yote, ile nuru kamili ya kweli? Ndugu Russell alijibu swali hilo waziwazi hivi: “Hakika sivyo; wala hatutakuwa nayo mpaka ule ‘mchana mkamilifu.’” (Mit. 4:18) Mara nyingi walirejezea imani za Kimaandiko walizokuwa nazo kuwa “kweli ya sasa”—si wakiwa na wazo la kwamba kweli yenyewe hubadilika bali kwa wazo la kwamba uelewevu wao juu yayo ulikuwa wenye kuendelea.
Hawa wanafunzi wa Biblia wenye moyo wa bidii hawakuepuka wazo la kwamba kuna jambo kama kweli katika mambo ya dini. Walitambua Yehova kuwa “Mungu wa kweli” na Biblia kuwa Neno lake la kweli. (Zab. 31:5; Yos. 21:45; Yn. 17:17) Walijua kwamba kulikuwa na mengi ambayo hawakujua, lakini hawakujizuia kusema kwa usadikisho yale waliyokuwa wamejifunza katika Biblia. Na wakati mafundisho na mazoea ya kidini ya kimapokeo yalipopingana na yale waliyopata yamesemwa waziwazi katika Neno la Mungu lililopuliziwa, basi, kwa kumwiga Yesu Kristo walifunua uwongo, hata ingawa kufanya hivyo kulileta dhihaka na chuki juu yao kutoka kwa makasisi.—Mt. 15:3-9.
-
-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Usadikisho katika Biblia nzima kuwa Neno la Mungu huendelea kuwa msingi wa imani za Mashahidi wa kisasa wa Yehova. Ulimwenguni pote, wana misaada ya kujifunza ambayo huwasaidia kuchunguza binafsi uthibitisho wa kupuliziwa kwayo. Pande za habari hiyo huzungumzwa mara nyingi katika magazeti yao. Katika 1969 walitangaza kitabu Is the Bible Really the Word of God? Miaka 20 baadaye kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? kilizungumzia tena habari ya uasilia wa Biblia, kilivuta fikira kwenye uthibitisho zaidi, na kikafikia mkataa uleule: Kwelikweli, Biblia ni Neno la Mungu lililopuliziwa. Kingine cha vitabu vyao, kilichochapwa kwanza katika 1963 na kupatanishwa na habari za karibuni zaidi katika 1990 (katika Kiingereza), ni “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa.” Habari nyingi zaidi zapatikana katika ensaiklopidia yao ya Biblia, Insight on the Scriptures, kilichotangazwa katika 1988.
Kutokana na funzo lao la kibinafsi na la kutaniko la habari kama hizo, wao wanasadikishwa kwamba ijapokuwa wanadamu kama 40 walitumiwa kuandika yale yaliyo katika vitabu 66 vya Biblia kwa pindi ya karne 16, kwa roho yake Mungu mwenyewe alielekeza kwa bidii uandikaji huo. Mtume Paulo aliandika: “Andiko lote limepuliziwa na Mungu.” (2 Tim. 3:16, NW; 2 Pet. 1:20, 21) Usadikisho huo ni jambo lenye nguvu katika maisha ya Mashahidi wa Yehova. Likitoa maelezo juu ya jambo hilo, gazeti la habari la Uingereza lilitaja hivi: “Kwa kila jambo analofanya Shahidi kuna sababu ya Kimaandiko. Kwa kweli, imani yao ya msingi ni kuitambua Biblia kuwa . . . ya kweli.”
-