-
Mashahidi wa YehovaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kwa kuwa Mashahidi wa Yehova wanategemeza imani zao zote, viwango vyao vya mwenendo, na taratibu za kitengenezo juu ya Biblia, imani yao katika Biblia yenyewe kuwa Neno la Mungu inawasadikisha kwamba wana kweli kabisa. Kwa hiyo msimamo wao si wa kujisifu bali unaonyesha uhakika wao kwamba Biblia ndiyo kiwango sahihi cha kupimia dini ya mtu. Wao si wenye ubinafsi bali wanatamani sana kushiriki imani zao pamoja na wengine.
-
-
Mashahidi wa YehovaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mashahidi wa Yehova huifafanua Biblia jinsi gani?
Jambo kuu ni kwamba Mashahidi wanaamini kabisa kwamba Biblia ni Neno la Mungu na kwamba yaliyomo ni ya kutufundisha. (2 Tim. 3:16, 17; Rom. 15:4; 1 Kor. 10:11) Kwa hiyo, hawatumii hoja za kifalsafa ili kuhepa maelezo yake ya kweli yaliyo wazi au kutetea njia ya maisha ya watu ambao wameacha viwango vyake vya maadili.
Wanapoeleza maana ya mifano katika Biblia, wao huiacha Biblia ijifafanue, badala ya kutoa maoni yao wenyewe. (1 Kor. 2:13) Mara nyingi, sehemu nyingine za Biblia huonyesha maana ya mifano hiyo. (Kwa mfano, ona Ufunuo 21:1; ndipo, kuhusu maana ya “bahari,” soma Isaya 57:20. Ili kumtambua “Mwana-Kondoo” anayetajwa katika Ufunuo 14:1, ona Yohana 1:29 na 1 Petro 1:19.)
Kuhusu kutimizwa kwa unabii, wanatumia maneno ya Yesu kuhusu kuwa macho ili kuona matukio yanayolingana na mambo aliyotabiri. (Luka 21:29-31; linganisha na 2 Petro 1:16-19.) Wanataja matukio hayo kwa uangalifu na kuelekeza fikira kwenye mambo ambayo Biblia inaonyesha kuwa maana yake.
Yesu alisema kwamba hapa duniani angekuwa na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” (kikundi cha wafuasi wake watiwa-mafuta), ambaye angemtumia kuandaa chakula cha kiroho kwa ajili ya watu wa nyumba ya imani. (Mt. 24:45-47) Mashahidi wa Yehova wanaukubali mpango huo. Kama Wakristo wa karne ya kwanza walivyokuwa, wao wanalitegemea baraza linaloongoza la jamii hiyo ya “mtumwa” kutatua maswali magumu—si kwa kutegemea hekima ya kibinadamu, bali kwa kutumia ujuzi wao wa Neno la Mungu na anavyowatendea watumishi wake, na kwa msaada wa roho ya Mungu, ambayo wanaomba kwa bidii.—Mdo. 15:1-29; 16:4, 5.
-