Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Una Haki ya Kuamini Utakalo
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Agosti 1
    • Mambo kama hayo yametokea kuhusiana na imani za kidini ambazo zinapingana sana. (1 Timotheo 4:1; 2 Timotheo 4:3, 4) Mtu fulani anaweza kuwa na imani yenye nguvu katika Mungu na mwingine aone imani hiyo kuwa ya upuuzi tu. Mtu fulani anasisitiza kwamba una nafsi isiyoweza kufa. Mwingine anaamini kwamba unapokufa, unakufa kabisa-kabisa, haundelei kuwa hai tena. Bila shaka, imani hizo zinazotofautiana haziwezi kuwa za kweli. Kwa hiyo, je, si jambo la hekima kuhakikisha kwamba jambo unaloamini ni la kweli na si kwa sababu tu unataka kuliamini? (Mithali 1:5) Unawezaje kufanya hivyo? Habari hiyo itachunguzwa katika makala ifuatayo.

  • Imani Yako Inategemea Nini?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Agosti 1
    • HATA HIVYO, kwa nini mtu atake kubadili dini au imani yake? Ni jambo la kawaida watu kusema kwamba “nina imani yangu, na ninaridhika nayo.” Hata wengi wanahisi kwamba imani isiyo ya kweli haiwezi kumdhuru mtu. Kwa mfano, mtu anayeamini kwamba dunia ni tambarare hawezi kudhuriwa na imani hiyo au kumdhuru mtu mwingine. Wengine husema “hatupaswi kubishana na wengine kwa sababu tu imani yao inatofautiana na yetu.” Je, hilo ni jambo la busara sikuzote? Je, daktari atakubaliana na mmoja wa wafanyakazi wenzake anayeamini kwamba ni sawa kugusa maiti kisha kwenda moja kwa moja kuwatibu wagonjwa kwenye wadi?

      Imani ya kidini isiyo ya kweli imesababisha madhara makubwa sana katika historia. Fikiria tisho lililotokea wakati viongozi wa kidini “walipowachochea Wakristo washupavu kutenda jeuri kwa ukatili” wakati wa mapambano yaliyoitwa Krusedi Takatifu za Enzi za Kati. Au wazia “Wakristo” wenye bunduki wa siku hizi ambao walipigana katika vita vya wenyewe kwa wenyewe hivi majuzi, na ambao ni “sawa na wapiganaji wa enzi za kati walioandika majina ya watakatifu kwenye panga zao, na kubandika picha za Bikira kwenye vitako vya bunduki zao.” Wakristo hao wote washupavu waliamini kwamba walikuwa wanafanya jambo lililo sawa. Hata hivyo, katika pambano hili na mapambano mengine ya kidini, kulikuwa na kasoro kubwa sana.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki