-
Nilivutiwa na Watu Wazee Wenye HekimaMnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
-
-
NILIPOKABILI MATATIZO
Baada ya kufurahia kazi ya mzunguko kwa miaka mitano, tulialikwa kutumika katika Betheli ya Uswisi. Nikiwa katika familia ya Betheli ya Uswisi, nilisisimuka kushirikiana na ndugu na dada wengi wazee walio wakomavu kiroho.
Muda mfupi baadaye, niligundua jambo lenye kushtua sana, kwamba mume wangu hakuwa mwaminifu kwangu wala kwa Yehova. Kisha akaniacha. Nilivurugika kabisa! Sidhani ningeweza kukabiliana na hali hiyo bila upendo na utegemezo wa marafiki wangu wapendwa wazee katika familia ya Betheli. Walinisikiliza nilipohitaji kuzungumza na waliniacha nipumzike nilipohitaji kupumzika. Maneno yao yenye kufariji na matendo yao ya fadhili yalinitegemeza nilipokuwa na maumivu makali sana na yalinisaidia kumkaribia Yehova hata zaidi.
-
-
Nilivutiwa na Watu Wazee Wenye HekimaMnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
-
-
[Picha katika ukurasa wa 15]
Elva akiwa na washiriki wa Betheli ya Uswisi mwaka wa 1960
-