-
“Wao Si Sehemu ya Ulimwengu”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Sikukuu hiyo iliadhimishwa kila mwaka hata na washiriki wa wafanyakazi wa makao makuu ya Watch Tower Society kwenye Kao la Betheli katika Brooklyn, New York. Kwa miaka mingi walikuwa wamejua kwamba Desemba 25 haikuwa tarehe sahihi, lakini wakatoa sababu kwamba kwa muda mrefu watu wengi walikuwa wameishirikisha tarehe hiyo na kuzaliwa kwa Mwokozi na kwamba kutendea wengine mema kwafaa siku yoyote. Hata hivyo, baada ya uchunguzi zaidi wa habari hiyo, washiriki wa wafanyakazi wa makao makuu ya Sosaiti, pamoja na wafanyakazi kwenye ofisi za tawi za Sosaiti katika Uingereza na Uswisi, waliamua kuacha kushiriki katika miadhimisho ya Krismasi, hivyo hakuna msherehekeo wa Krismasi uliofanywa huko baada ya 1926.
-
-
“Wao Si Sehemu ya Ulimwengu”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 200, 201]
Mazoea Ambayo Yameachwa Kabisa
Msherehekeo huu wa Krismasi kwenye Betheli ya Brooklyn katika 1926 ulikuwa ndio wao wa mwisho. Wanafunzi wa Biblia walikuja kufahamu hatua kwa hatua kwamba wala mwanzo wa sikukuu hiyo wala mazoea yaliyoshirikishwa nayo hayakumheshimu Mungu
-