-
‘Tumefanya Lile Tulilopaswa Kufanya’Mnara wa Mlinzi—1998 | Agosti 1
-
-
Ninaamini kwamba kuna masomo mengi ambayo familia zaweza kujifunza kutokana na vile ambavyo Betheli huendesha shughuli zake. Sisi huamka asubuhi na mapema na kuanza siku kwa mambo ya kiroho kwa kuchunguza andiko la Biblia la kila siku. Tunatarajiwa kufanya kazi kwa bidii na kuishi maisha yenye usawaziko lakini yenye shughuli nyingi. Betheli sio kama nyumba ya watawa, kama vile ambavyo wengine huenda wakafikiri. Tunatimiza mengi kwa sababu ya njia yetu ya maisha yenye utaratibu. Wengi wamesema kwamba mazoezi waliyopokea Betheli yaliwasaidia baadaye kukubali madaraka katika familia zao na katika kutaniko la Kikristo.
Huenda wanaume na wanawake vijana wanaokuja Betheli wakapewa mgawo wa kusafisha, udobi, au mgawo wa kufanya kazi katika kiwanda. Huenda ulimwengu ukataka tuamini kwamba kazi ngumu kama hiyo inatushushia heshima na hatustahili kuifanya. Hata hivyo, vijana katika Betheli huja kuthamini kwamba migawo hiyo ya kazi ni ya lazima ili familia yetu iendeshe shughuli zake ifaavyo na kwa furaha.
Huenda ulimwengu pia ukaendeleza wazo la kwamba unahitaji cheo na fahari ili kuwa mwenye furaha kikweli. Si sawa kuwaza hivyo. Tufanyapo kazi ambayo tumegawiwa, huwa ‘tunafanya tunalopaswa kufanya,’ nasi hupokea baraka za Yehova. (Luka 17:10) Tunaweza kuwa na uradhi na furaha halisi tukikumbuka tu kusudi la kazi yetu ambalo ni kufanya mapenzi ya Yehova na kuendeleza masilahi ya Ufalme. Tukikumbuka mambo hayo, mgawo wowote ule unaweza kuwa wenye kufurahisha na kuridhisha.
-
-
‘Tumefanya Lile Tulilopaswa Kufanya’Mnara wa Mlinzi—1998 | Agosti 1
-
-
Masomo Ambayo Nimejifunza
Nimejifunza kwamba mwangalizi mzuri ni yule awezaye kupata habari yenye thamani kutoka kwa wengine. Maoni yaliyo mengi ambayo nimependelewa kutumia nikiwa mwangalizi wa Betheli yametokana na wengine.
Nilipokuja Betheli, wengi walikuwa na umri mkubwa zaidi, kama nilivyo leo. Wengi sasa hawako. Ni nani ambaye huchukua mahali pa wanaozeeka na kufa? Sikuzote si wale wenye uwezo zaidi. Bali ni wale wanaopatikana, wanaofanya kazi kwa uaminifu na wanaojitoa.
Jambo jingine la maana kukumbukwa ni thamani ya mke mwema. Utegemezo wa Fern, mke wangu mpendwa, umenisaidia sana kutimiza migawo yangu ya kitheokrasi. Waume wana daraka la kuhakikisha kwamba wake zao wanafurahia migawo yao. Huwa ninajaribu kupanga jambo fulani ambalo Fern nami hupenda kufanya. Si lazima liwe jambo lenye gharama kubwa, bali ni jambo tofauti na yale sisi hufanya kila siku. Ni jukumu la mume kufanya mambo ili kumfurahisha mke wake. Wakati anaotumia pamoja naye ni wenye thamani na hupita haraka, kwa hiyo anahitaji kuutumia vizuri kabisa.
Ninafurahi kuishi katika siku za mwisho ambazo Yesu alizungumzia. Huu ndio wakati wenye kustaajabisha zaidi katika historia yote ya kibinadamu. Tunaweza kuangalia na kuona kwa macho yetu ya imani jinsi Bwana anavyolisitawisha tengenezo lake ili liwe tayari kwa ajili ya kufika kwa ulimwengu mpya ulioahidiwa. Nikumbukapo maisha yangu nikiwa katika utumishi wa Yehova, ninaweza kuona kwamba Yehova ndiye anayeongoza tengenezo hili—si wanadamu. Sisi ni watumishi wake tu. Na tukiwa watumishi wake, ni lazima sikuzote tumtegemee kupata mwongozo. Mara atuelezapo yale tupaswayo kufanya, twapaswa kuwa tayari kutii na kuwa wenye ushirikiano.
Shirikiana kikamili na tengenezo, na unahakikishiwa kuwa na maisha kamili yenye furaha. Lolote lile ufanyalo—liwe ni upainia, kazi ya kuzunguka, kutumikia kutanikoni ukiwa mhubiri, utumishi wa Betheli au kazi ya umishonari—fuata mwongozo unaotolewa, na thamini mgawo wako. Jaribu kadiri uwezavyo kufurahia kila mgawo na pia kila siku ufanyayo kazi katika utumishi wa Yehova. Utachoka, na huenda ukafanya kazi kupita kiasi au nyakati nyingine ukavunjika moyo. Huo ndio wakati ambapo inakubidi ukumbuke kusudi la kuweka maisha yako wakfu kwa Yehova. Ni kufanya mapenzi yake, si yako mwenyewe.
Hakuna siku ambayo nimekuja kazini nisifurahie nilichofanya. Kwa nini? Kwa sababu tunapojitoa kwa Yehova kwa nafsi yote, tunapata uradhi wa kujua kwamba ‘tumefanya lile tulilopaswa kufanya.’
-