Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Waweza Kujitolea?
    Huduma ya Ufalme—2001 | Juni
    • 6 Matakwa ya Utumishi wa Betheli: Inafaa wale wanaoomba kutumikia Betheli wawe tayari kufanya kazi kwa bidii, si kuwa “wenye kuzipenda raha.” (2 Tim. 3:4; 1 Kor. 13:11) Washiriki wa familia ya Betheli wanapaswa kuwa wanaume na wanawake wa kiroho ambao wamesitawisha mazoea mazuri ya funzo la kibinafsi na wamezoeza nguvu zao za kufikiri ili “kutofautisha lililo sahihi na lililo kosa pia.” (Ebr. 5:14) Ukomavu wao wa Kikristo wapaswa kuwa tayari umeonyeshwa katika sehemu zote za maisha, kutia ndani mavazi, mapambo, na uchaguzi wao wa muziki na tafrija. Washiriki wa familia ya Betheli wako tayari kutumikia popote wanapohitajiwa. Mara nyingi washiriki vijana hupewa migao inayohusu kazi ya kutumia nguvu za kimwili, kutia ndani uchapaji, kutayarisha na kutuma vichapo, udumishaji, utunzaji wa vyumba, usafi, udobi, na kupika. (Mit. 20:29) Ingawa hivyo, tofauti na kazi ya kuajiriwa, kila mgao huleta uradhi kwa sababu ni utumishi mtakatifu unaomletea Yehova utukufu.—Kol. 3:23.

      7 Kwa kawaida, wale wanaoitwa Betheli huhitajiwa kukaa huko kwa angalau mwaka mmoja ili waweze kuzoezwa kuwa wafanyakazi wenye matokeo. Inatumainiwa kwamba wataweza kukaa Betheli. Upendo kwa Yehova ndio huwachochea washiriki wa familia ya Betheli kutanguliza kazi ya Ufalme badala ya mambo yao ya kibinafsi, jambo ambalo lampendeza Yehova.—Mt. 16:24.

  • Je, Waweza Kujitolea?
    Huduma ya Ufalme—2001 | Juni
    • Kwa sababu ya namna ya kazi inayofanywa Betheli, uhitaji wetu mkubwa kwa sasa ni wa akina ndugu waseja. Ijapokuwa si takwa, wale wanaopewa nafasi ya kwanza ni mapainia wa kawaida, kwa kuwa tayari wako katika utumishi wa wakati wote. Wakati mwingine dada waseja na wenzi waliooana wenye umri wa miaka 19 hadi 35 ambao huenda wakawa na ustadi fulani unaohitajiwa Betheli, wanaweza kuitwa. Kwa kuongezea, akina ndugu na dada ambao wamepita umri wa miaka 35 na wana ustadi na mazoezi ya pekee ambayo yanaweza kutumika Betheli wanatiwa moyo kujaza fomu ya ombi. Kwa mfano hao wanatia ndani madaktari wa meno, madaktari wa kawaida, wajuzi wa hesabu waliopata cheti, wahandisi, wauguzi waliosajiliwa, mekanika wa magari, au mafundi wa umeme. Hata hivyo, hatuwatii moyo watu wakapate elimu ya pekee kwa kuwazia kwamba hiyo itaongeza uwezekano wao wa kuitwa Betheli. Wale ambao tayari walipokea mazoezi ya pekee labda kabla ya kuingia katika kweli, wanaweza kuandika muhtasari wa mambo hayo na kuunganisha muhtasari huo pamoja na fomu ya ombi la Betheli.

  • Je, Waweza Kujitolea?
    Huduma ya Ufalme—2001 | Juni
    • 14 Wale Wanaotumikia Betheli Lazima Wawe Safi Kiadili: Mtunga-zaburi aliuliza: “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake?” Alijibu hivi: “Kwa kutii, akilifuata neno [la Yehova].” (Zab. 119:9) Hilo latia ndani kuepuka kufisidiwa na ulimwengu wa Shetani. Ponografia ya Internet, mwenendo usiofaa pamoja na watu wa jinsia tofauti, muziki wenye kushusha heshima, vitumbuizo visivyofaa na kunywa vileo kabla ya umri unaokubaliwa ni baadhi ya mitego anayotumia Shetani ili kuwazuia vijana wetu wasifikie miradi ya kiroho. Azimio lenye nguvu lahitajiwa ili kukinza mbinu hizo. Kama kijana, ikiwa wajipata unahusika na yoyote ya mambo haya, zungumza na wazee katika kutaniko lenu na utatue mambo hayo kabla ya kuomba kutumikia Betheli. Kuwa na dhamiri njema ni muhimu ili kumtumikia Yehova kikamili.—1 Tim. 1:5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki