-
BibliaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Neno la Yehova Mungu lililoandikwa kwa ajili ya binadamu.
-
-
BibliaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Sehemu kubwa ya maandishi hayo ina maneno ya Yehova mwenyewe pamoja na habari kuhusu mafundisho na utendaji wa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu. Humo tunapata matakwa ya Mungu kwa watumishi wake na yale atakayofanya ili atimize kusudi lake kuu kwa ajili ya dunia. Ili kutusaidia kuyathamini mambo hayo, Yehova pia alihifadhi katika Biblia maandishi yanayoonyesha mambo ambayo humpata mtu mmoja-mmoja na mataifa wanapomsikiliza Mungu na kutenda kupatana na kusudi lake, pia yale yanayotokea wanapofuata njia zao wenyewe. Kupitia maandishi hayo ya kihistoria yenye kutegemeka Yehova anatufahamisha jinsi anavyoshughulika na wanadamu na hivyo kutufahamisha utu wake mwenyewe ulio mzuri ajabu.
-