-
Tumia kwa Ustadi “Upanga wa Roho”Mnara wa Mlinzi—2010 | Februari 15
-
-
8, 9. Ni nini kitakachotusaidia kuelewa Biblia? Toa mfano.
8 Ni nini kitakachotusaidia ‘kulitumia sawasawa neno la kweli’ katika huduma yetu? Kabla ya kuwasaidia wengine waelewe vizuri mafundisho ya Biblia, sisi wenyewe tunahitaji kuyaelewa vizuri. Kwa hiyo, ni lazima tuchunguze muktadha wa andiko au mistari fulani. Kamusi moja inasema kwamba “muktadha wa neno, sentensi, au andiko ni maneno, sentensi mbalimbali, au maandishi yanayotangulia na yale yanayofuata neno hilo, andiko au sentensi hiyo, ambayo yanatusaidia kuelewa waziwazi maana yake.”
9 Ili kuelewa Andiko fulani kwa usahihi tunahitaji kuchunguza mistari inayozunguka andiko hilo. Kwa mfano, tunahitaji kuchunguza muktadha ili kuelewa maneno ya Paulo kwenye Wagalatia 5:13. Aliandika hivi: “Bila shaka, ninyi mliitiwa uhuru, akina ndugu; ila msiutumie uhuru huu kuuchochea mwili, bali kupitia upendo mtumikiane.” Katika andiko hilo, Paulo alikuwa akizungumza kuhusu uhuru gani? Je, ni uhuru kutoka katika dhambi na kifo, uhuru kutoka katika dini ya uwongo, au uhuru wa aina nyingine? Mistari inayozunguka mstari huo inaonyesha kwamba Paulo alikuwa akizungumza kuhusu ‘kuachiliwa huru kutoka katika laana ya Sheria.’ (Gal. 3:13, 19-24; 4:1-5) Alikuwa akizungumza kuhusu uhuru wa Kikristo. Watu waliothamini uhuru huo walitumikiana kwa upendo. Wale ambao hawakuwa na upendo waligombana na kuwasengenya wengine.—Gal. 5:15.
10. Ili kuelewa maana ya Maandiko kwa usahihi, tunapaswa kuchunguza habari gani, na tunaweza kuzipata jinsi gani?
10 Neno “muktadha” lina maana nyingine. Linamaanisha pia ‘mazingira au hali ambamo tukio au jambo linatendeka.’ Ili kuelewa maana ya andiko kwa usahihi, tunapaswa kuchunguza mazingira ya masimulizi hayo, kwa mfano, ni nani aliyeandika kitabu hicho cha Biblia na kiliandikwa wakati gani, na katika hali gani? Ni jambo la maana pia kujua kitabu hicho kiliandikwa kwa sababu gani na ikiwezekana, hali za kijamii, kimaadili, na mazoea ya kidini yaliyokuwapo wakati kilipoandikwa.a
-
-
Tumia kwa Ustadi “Upanga wa Roho”Mnara wa Mlinzi—2010 | Februari 15
-
-
a Unaweza kupata habari mbalimbali kuhusu vitabu vya Biblia katika kitabu “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa,” mabuku ya Insight on the Scriptures (Étude perspicace des Écritures), na makala kama vile “Neno la Yehova Liko Hai,” katika Mnara wa Mlinzi.
-