Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Twatambuliwa kwa Mwenendo Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • “Tabia au Agano—Jipi Kati ya Hayo?”

      Ingawa walianza kwa shauri thabiti la Kimaandiko juu ya uhitaji wa kuwa kama Kristo, mkazo ambao baadhi ya Wanafunzi wa Biblia wa mapema walitia katika “kusitawisha tabia,” kama walivyokuita, ulielekea kupunguza pande fulani za Ukristo wa kweli. Baadhi yao walionekana wakiwa na maoni ya kwamba kuwa muungwana—kuonekana sikuzote kuwa mwenye fadhili na mwema, kusema kwa sauti pole, kuepuka wonyesho wowote wa hasira, kusoma Maandiko kila siku—kungewahakikishia kuingia mbinguni. Lakini hao walikosa kuona uhakika wa kwamba Kristo alikuwa amewapa wafuasi wake kazi ya kufanya.

      Tatizo hilo lilizungumzwa kwa uthabiti katika makala “Tabia au Agano—Jipi Kati ya Hayo?” katika toleo la Mei 1, 1926, la The Watch Tower.a Ilionyesha kwamba jitihada za kusitawisha “tabia kamilifu” wakati wa kuwa katika mwili zilifanya wengine waache kujitahidi kwa sababu ya kuvunjika moyo, bali wakati uleule, zikitokeza katika wengine mtazamo wa kujitakia uadilifu na zikaelekea kuwafanya wakose kuona thamani ya dhabihu ya Kristo. Baada ya kukazia imani katika damu ya Kristo iliyomwagwa, makala hiyo ilikazia umaana wa ‘kufanya mambo’ katika utumishi wenye utendaji wa Mungu ili kutoa uthibitisho kwamba mtu alikuwa akifuatia mwendo wenye kumpendeza Mungu. (2 Pet. 1:5-10) Wakati huo, ambapo sehemu kubwa ya Jumuiya ya Wakristo ilikuwa ingali ikijisingizia kushikamana na viwango vya adili vya Biblia, mkazo huo juu ya utendaji uliimarisha ile tofauti iliyokuwako kati ya Mashahidi wa Yehova na Jumuiya ya Wakristo. Tofauti hiyo ilipata kuwa wazi hata zaidi kadiri masuala ya kiadili ambayo yalikuwa yakiwa ya kawaida yalikuwa lazima yashughulikiwe na wote waliodai kuwa Wakristo.

  • Twatambuliwa kwa Mwenendo Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku katika ukurasa wa 173]

      ‘Kusitawisha Tabia’—Tunda Halikuwa Zuri Sikuzote

      Ripoti moja kutoka Denmark: ‘Wengi, hasa miongoni mwa akina ndugu wa umri mkubwa zaidi, katika jitihada zao za moyo mweupe za kuvaa utu wa Kikristo, walijitahidi kuepuka kila kitu kilichofanana kidogo sana na tabia ya ulimwengu ili kwa njia hiyo wajistahilishe Ufalme wa kimbingu. Mara nyingi, lilifikiriwa kuwa jambo lisilofaa kutabasamu wakati wa mikutano, na wengi wa akina ndugu wenye umri mkubwa zaidi walivaa suti nyeusi, viatu vyeusi, tai nyeusi tu. Mara nyingi walitosheka kuishi maisha matulivu na ya amani katika Bwana. Waliamini kwamba ilitosha kufanya mikutano na kuacha makolpota wafanye kazi ya kuhubiri.’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki