Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wao Si Sehemu ya Ulimwengu”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Sikukuu hiyo iliadhimishwa kila mwaka hata na washiriki wa wafanyakazi wa makao makuu ya Watch Tower Society kwenye Kao la Betheli katika Brooklyn, New York. Kwa miaka mingi walikuwa wamejua kwamba Desemba 25 haikuwa tarehe sahihi, lakini wakatoa sababu kwamba kwa muda mrefu watu wengi walikuwa wameishirikisha tarehe hiyo na kuzaliwa kwa Mwokozi na kwamba kutendea wengine mema kwafaa siku yoyote. Hata hivyo, baada ya uchunguzi zaidi wa habari hiyo, washiriki wa wafanyakazi wa makao makuu ya Sosaiti, pamoja na wafanyakazi kwenye ofisi za tawi za Sosaiti katika Uingereza na Uswisi, waliamua kuacha kushiriki katika miadhimisho ya Krismasi, hivyo hakuna msherehekeo wa Krismasi uliofanywa huko baada ya 1926.

      R. H. Barber, mshiriki wa wafanyakazi wa makao makuu aliyefanya uchunguzi kamili wa chanzo cha desturi za Krismasi na tunda zilizokuwa zikizaa, alitoa matokeo yake katika tangazo la redio. Habari hiyo ilitangazwa pia katika The Golden Age la Desemba 12, 1928. Ulikuwa mfichuo kamili wa mianzo yenye kumvunjia Mungu heshima ya Krismasi. Tangu hapo, mianzo ya kipagani ya desturi za Krismasi imepata kujulikana na umma kwa ujumla, lakini ni watu wachache ambao hufanya mabadiliko katika njia yao ya maisha likiwa tokeo. Kwa upande ule mwingine, Mashahidi wa Yehova wana nia ya kufanya mabadiliko yanayohitajiwa ili wawe wenye kukubalika zaidi wakiwa watumishi wa Yehova.

      Walipoonyeshwa kwamba kuzaliwa kwa Yesu kulikuwa kumekuwa kwenye kupendeza zaidi watu wengi kuliko fidia iliyoandaliwa na kifo chake; kwamba kelele za ulevi za sikukuu hiyo na roho ambayo zawadi nyingi zilitolewa hazimheshimu Mungu; kwamba wale wanajimu ambao kutoa zawadi kwao kulikuwa kukiigwa walikuwa kwa kweli wanajimu walioongozwa na mashetani; kwamba wazazi walikuwa wakiwawekea watoto wao kielelezo cha kusema uwongo kwa yale waliyowaambia juu ya Baba Krismasi; kwamba “Mtakatifu Nikolasi” (Baba Krismasi) kwa kweli lilikuwa jina jingine la Ibilisi mwenyewe; na kwamba miadhimisho hiyo ilikuwa, kama vile alivyokiri Kardinali Newman katika kitabu chake Essay on the Development of Christian Doctrine, “vyombo na nyongeza hasa za ibada ya mashetani” ambazo kanisa lilikuwa limekubali—walipojulishwa mambo hayo, Mashahidi wa Yehova waliacha mara hiyo na kwa daima kushiriki sehemu yoyote katika misherehekeo ya Krismasi.

  • “Wao Si Sehemu ya Ulimwengu”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 200, 201]

      Mazoea Ambayo Yameachwa Kabisa

      Msherehekeo huu wa Krismasi kwenye Betheli ya Brooklyn katika 1926 ulikuwa ndio wao wa mwisho. Wanafunzi wa Biblia walikuja kufahamu hatua kwa hatua kwamba wala mwanzo wa sikukuu hiyo wala mazoea yaliyoshirikishwa nayo hayakumheshimu Mungu

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki