Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Baadaye, baada ya yeye mwenyewe kuwa amejionea yale ambayo kwa kweli Biblia hufundisha, alinukuliwa na mmoja wa washirika wake kuwa alitaarifu hivi: “Ikiwa Biblia inafundisha kwamba mateso ya milele ndiyo hukumu ya wote isipokuwa watakatifu, yapasa kuhubiriwa—naam, kwa sauti kuu ili wote wasikie, kila juma, kila siku, kila saa; ikiwa haifundishi hivyo, uhakika huo wapasa kujulishwa, na doa baya lenye kuvunjia heshima jina takatifu la Mungu liondolewe.”

      Kwenye hatua ya mapema ya funzo lake la Biblia, C. T. Russell aliona waziwazi kwamba helo (kuzimu) si mahali pa mateso ya nafsi baada ya kifo. Yaelekea sana alisaidiwa katika jambo hilo na George Storrs, mhariri wa Bible Examiner, ambaye Ndugu Russell alimtaja kwa uthamini mchangamfu katika maandishi yake na ambaye yeye mwenyewe aliandika mengi juu ya yale aliyotambua katika Biblia kuwa ndiyo hali ya wafu.

  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kulielekeza “Bomba la Maji” Kwenye Helo

      Kwa kupatana na tamaa yenye nguvu ya Ndugu Russell ya kuondolea jina la Mungu doa baya lililotokana na fundisho la moto wa helo wenye mateso ya milele, yeye aliandika trakti iliyozungumzia habari, “Je, Maandiko Hufundisha Kwamba Mateso ya Milele Ndiyo Mshahara wa Dhambi?” (The Old Theology, 1889) Humo alisema hivi:

      “Nadharia ya mateso ya milele ilikuwa na chanzo cha kipagani ingawa kama ilivyoaminiwa na wapagani haikuwa fundisho lisilo la huruma kama vile ilivyopata kuwa baadaye, ilipoanza kujishikamanisha hatua kwa hatua na Ukristo wa jina tu wakati huo ulipochanganyana na falsafa za kipagani katika karne ya pili. Ilibaki juu ya uasi-imani mkubwa kubandika kwenye falsafa ya kipagani yale mambo mengi yenye kuogofya yanayoaminiwa sana sasa kwa ujumla, kuyachora kwenye kuta za makanisa, kama ilivyofanywa katika Ulaya, kuyaandika katika taarifa za imani zao na katika nyimbo zao za kidini, na kulipotoa sana Neno la Mungu ili kulipa kufuru hilo lenye kumvunjia Mungu heshima lile linaloonekana kuwa uungaji mkono wa kimungu. Kwa hiyo, ile imani ya kisasa isiyo na uthibitisho, huipokea ikiwa urithi, si kutoka kwa Bwana, wala mitume, wala manabii, bali kutoka kwa ile roho ya kuridhiana iliyodhabihu kweli na kusababu kuzuri, ikapotoa kwa njia ya aibu mafundisho ya Ukristo kwa kuwa na tamaa ya makuu isiyo takatifu na ugomvi juu ya mamlaka na mali na idadi za watu. Mateso ya milele yakiwa adhabu ya dhambi, mjeledi ambao wale wenye kuamini bila uthibitisho, wale wasiojua kitu na wenye ushirikina wa ulimwengu wamepigwa kwao ili watii ukatili kitumwa—hayakujulikana kwa wazee wa ukoo wa enzi zilizopita; hayakujulikana kwa manabii wa enzi ya Kiyahudi na hayakujulikana kwa Bwana na mitume; bali yamekuwa ndiyo fundisho kuu la Ukristo wa Jina tangu ule uasi-imani mkubwa. Mateso ya milele yalitangazwa kwa wote waliokinza au waliopuuza mamlaka ya Kanisa la Roma, na kupasishwa kwayo katika maisha haya kulianza kwa kadiri Kanisa la Roma lilivyokuwa na nguvu.”

      Ndugu Russell alifahamu sana kwamba wengi zaidi kati ya watu wenye akili hawakuamini kikweli fundisho la moto wa helo. Lakini, kama vile alivyotaja, katika 1896, katika kijitabu What Say the Scriptures About Hell?, “kwa kuwa wao hufikiri kwamba Biblia hulifundisha, kila hatua ya maendeleo wafanyayo katika akili ya kweli na fadhili ya kidugu . . . katika visa vingi zaidi ni hatua ya kwenda mbali na Neno la Mungu, ambalo wao hushtakia fundisho hilo kwa uwongo.”

      Ili kuwavuta watu kama hao wenye kufikiri warudie Neno la Mungu, yeye alitoa katika kijitabu hicho kila andiko katika King James Version ambamo neno helo lilipatikana, ili wasomaji waweze kujionea wenyewe yale ambayo hayo yalisema, na kisha akataarifu hivi: “Twashukuru Mungu, hatupati mahali kama hapo pa mateso ya milele kama inavyofundishwa kimakosa na taarifa za imani za kidini, na vitabu vya nyimbo za kidini, na mimbari. Hata hivyo tumepata ‘helo,’ sheoli, hadesi, ambamo jamii yetu yote ilihukumiwa kwenda kwa sababu ya dhambi ya Adamu, na ambamo wote watoka kwa kukombolewa na kifo cha Bwana yetu; na ‘helo’ hiyo ni ziara—hali ya kifo. Na sisi twapata ‘helo’ nyingine (gehena—kile kifo cha pili—uharibifu kabisa) iliyoletwa kwenye uangalifu wetu ikiwa adhabu ya mwisho juu ya wote ambao, baada ya kukombolewa na kuletwa kwenye ujuzi kamili wa kweli, na kwenye uwezo kamili wa kuutii, bado watachagua kifo kwa kuchagua mwendo wa kupinga Mungu na uadilifu. Na mioyo yetu yasema, Amina. Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa. Ni nani asiyekucha, Ee Bwana na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako u mtakatifu kabisa. Na mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo yako ya haki yamedhihirishwa.”—Ufu. 15:3, 4.

      Aliyokuwa akifundisha yalikuwa chanzo cha udhia na aibu kwa makasisi wa Jumuiya ya Wakristo. Katika 1903 alitolewa mwito wa kushindana kwenye mjadala wa hadhara. Hali ya wafu lilikuwa mojapo masuala katika mfululizo uliotokea wa mijadala kati ya C. T. Russell na Dakt. E. L. Eaton aliyetumikia akiwa msemaji wa muungano usio rasmi wa wahudumu Waprotestanti katika sehemu ya magharibi ya Pennsylvania.

      Wakati wa mijadala hiyo Ndugu Russell alitegemeza imara hoja ya kwamba “kifo ni kifo, na kwamba wapendwa wetu, wafapo, kwa kweli wamekufa, kwamba hawako hai wala pamoja na malaika wala pamoja na roho waovu katika mahali pasipo na tumaini.” Ili kuunga mkono hilo, yeye alirejezea maandiko kama vile Mhubiri 9:5, 10; Warumi 5:12; 6:23; na Mwanzo 2:17. Yeye alisema hivi pia: “Maandiko yanapatana kabisa na yale ambayo wewe na mimi na mtu mwingine yeyote mwenye akili timamu, mwenye kusababu ifaavyo katika ulimwengu atakubali kuwa ndio utu wenye kupatana na akili na wenye kufaa wa Mungu wetu. Ni nini lijulishwalo kuhusu Baba yetu wa mbinguni? Kwamba yeye ni mwenye haki, kwamba yeye ni mwenye hekima, kwamba yeye ni mwenye upendo, kwamba yeye ni mwenye nguvu. Watu wote Wakristo watakiri sifa hizo za utu wa kimungu. Ikiwa ni hivyo, je, sisi twaweza kupata maana yoyote ya neno ambamo tungeweza kumfikiria Mungu kuwa mwenye haki na bado aadhibu kiumbe [aliyeumbwa kwa] mkono Wake kwa umilele wote, haidhuru dhambi yake ilikuwa nini? Mimi si mteteaji wa dhambi; wala siishi katika dhambi mimi mwenyewe, na mimi sihubiri dhambi kamwe. . . . Lakini nakuambia kwamba watu hawa wote waliopo hapa ambao ndugu yetu [Dakt. Eaton] asema wanasema bila staha kwa makufuru yao kwa Mungu na jina takatifu la Yesu Kristo wote ni watu ambao wamefundishwa fundisho hilo la mateso ya milele. Na wauaji-kimakusudi, wevi na watenda maovu wote waliomo gerezani, wote walifundishwa fundisho hilo. . . . Hayo ni mafundisho mabaya; yamekuwa yakidhuru ulimwengu kwa muda wote huu; hayo si sehemu ya fundisho la Bwana hata kidogo, na uwezo wa kuona wa kiroho wa ndugu yetu mpendwa ungali una giza.”

      Inaripotiwa kwamba baada ya mjadala huo, kasisi mmoja aliyehudhuria alimwendea Russell na kusema: “Naterema kuona ukielekeza bomba la maji kwenye helo na kuuzima moto huo.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki