Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ule Umati Mkubwa Kuishi Mbinguni? Au Duniani?
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Miaka mingine 60 ilipita kabla mtume Yohana hajafunuliwa kwamba ni 144,000 tu ambao wangechukuliwa kutoka duniani kushiriki Ufalme wa kimbingu pamoja na Kristo.—Ufu. 7:4-8; 14:1-3.

      Charles Taze Russell na washirika wake walishiriki tumaini hilo, kama vile walio wengi kati ya Mashahidi wa Yehova kuteremka hadi miaka ya katikati ya 1930. Walijua pia, kutokana na funzo lao la Maandiko, kwamba kutiwa mafuta kwa roho takatifu hakukuonyesha tu kwamba watu walikuwa katika hali ya kupokea utumishi wa wakati ujao wakiwa wafalme na makuhani pamoja na Kristo mbinguni, bali pia kwamba walikuwa na kazi ya pekee ya kufanya wakati wangali katika mwili. (1 Pet. 1:3, 4; 2:9; Ufu. 20:6) Kazi gani? Walijua vizuri na mara nyingi walinukuu andiko la Isaya 61:1 ambalo hutaarifu hivi: “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu BWANA amenitia mafuta, niwahubiri wanyenyekevu habari njema.”

  • Ule Umati Mkubwa Kuishi Mbinguni? Au Duniani?
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Waling’amua kwamba, wakati ule, ni “mwito” mmoja tu uliokuwa ukitolewa kwa Wakristo wote wa kweli. Huo ulikuwa mwaliko wa kuwa washiriki wa bibi-arusi wa Kristo, ambaye hatimaye angekuwa na hesabu ya 144,000 tu. (Efe. 4:4; Ufu. 14:1-5) Walijitahidi kuwachochea wawe watendaji wale wote waliodai kuwa na imani katika dhabihu ya fidia ya Kristo, wawe walikuwa washiriki wa kanisa au la, ili wathamini “ahadi zenye bei na zilizo bora sana” za Mungu. (2 Pet. 1:4; Efe. 1:18, NW) Walijitahidi kuwachochea wawe na bidii katika kujipatanisha na matakwa ya kuwa kundi dogo la warithi wa Ufalme. Kwa ajili ya kuimarisha kiroho wote hao, ambao waliona kuwa washiriki wa “watu wa nyumba ya imani” (kwa sababu walidai kuwa na imani katika fidia), Ndugu Russell na washirika wake walijitahidi kwa bidii kufanya ‘chakula cha kiroho kwa wakati ufaao’ kipatikane kupitia safu za Watch Tower na vichapo vingine vyenye msingi wa Biblia.—Gal. 6:10; Mt. 24:45, 46, KJ.

      Hata hivyo, wangeweza kuona kwamba si wote waliodai kuwa “wamejitakasa” (au, ‘kuwa wamejitoa wenyewe kikamili kwa Bwana,’ kama vile walivyolielewa kuwa lamaanisha) waliendelea baada ya hapo kufuatia maisha ya kujidhabihu kwa nia, wakifanya utumishi wa Bwana kuwa hangaiko lao la kwanza maishani. Hata hivyo, kama vile walivyoeleza, Wakristo waliojitakasa walikuwa wamekubali kuacha kwa nia asili yao ya kibinadamu, kwa kutazamia urithi wa kimbingu; hakukuwa cha kurudi nyuma; ikiwa hawakupata uhai katika makao ya kiroho, kifo cha pili kingewangoja. (Ebr. 6:4-6; 10:26-29) Lakini Wakristo wengi walioonekana kuwa wamejitakasa walikuwa wakichukua ile njia rahisi, wakishindwa kuonyesha bidii ya kweli kwa ajili ya kazi ya Bwana na wakiepuka kujidhabihu. Hata hivyo, kwa wazi hawakuwa wameikana fidia na walikuwa wakiishi maisha safi kadiri. Ingekuwaje kwa watu kama hao?

      Kwa miaka mingi Wanafunzi wa Biblia walifikiri kwamba hicho ndicho kile kikundi kilichoelezwa kwenye Ufunuo 7:9, 14 (KJ), ambao hurejezea “halaiki kubwa” itokayo katika ile dhiki kubwa na kusimama “mbele ya kiti cha ufalme” cha Mungu na mbele za Mwana-Kondoo, Yesu Kristo. Walitoa sababu kwamba ijapokuwa hao huepuka maisha ya kujidhabihu, wangekabiliwa na majaribu ya imani yakimalizikia kwenye kifo wakati wa dhiki baada ya kutukuzwa kwa wale wa mwisho wa bibi-arusi wa Kristo. Waliamini kwamba ikiwa hao waliosemekana kuwa wa halaiki kubwa walikuwa waaminifu wakati huo, wangefufuliwa kwenye uhai wa kimbingu—si kutawala wakiwa wafalme bali ili kuchukua msimamo wao mbele ya kiti cha ufalme. Sababu ilitolewa kwamba wangepewa vyeo hivyo vya pili kwa sababu upendo wao kwa Bwana haukuwa umewaka vya kutosha, kwa sababu hawakuwa wameonyesha bidii ya kutosha. Ilifikiriwa kwamba wao walikuwa watu ambao walikuwa wamezaliwa kwa roho ya Mungu lakini walikuwa wamepuuza kumtii Mungu, labda wakiendelea kushikamana na makanisa ya Jumuiya ya Wakristo.

      Pia walidhani kwamba labda—labda tu—wale “wakuu wa kale” ambao wangetumikia wakiwa wakuu duniani wakati wa enzi ya mileani, mwishoni mwa wakati huo, wangepewa kwa njia fulani uhai wa kimbingu. (Zab. 45:16) Walitoa sababu kwamba mataraja kama hayohayo huenda yangengoja wowote ambao “walijitakasa” baada ya warithi wa Ufalme wote 144,000 kuwa wamechaguliwa hatimaye lakini kabla ya wakati wa urudisho kuanza duniani. Kwa kadiri ndogo, hayo yalikuwa maoni yaliyotolewa katika Jumuiya ya Wakristo ya kwamba wale wote walio wema vya kutosha huenda mbinguni.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki