-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Mwaka uliofuata, katika kujibu swali, “Je, nyinyi mwadai kwamba Biblia haifundishi kwamba kuna watu watatu katika Mungu mmoja?” jibu lililotolewa ni: “Ndiyo: Tofauti na hilo, [Biblia] hutuambia kwamba kuna Mungu mmoja na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo ambaye vitu vyote vyatoka kwake (au aliyeumba vitu vyote). Basi sisi twaamini katika Mungu na Baba Mmoja, na pia katika Bwana mmoja Yesu Kristo . . . Lakini hao ni wawili wala si mtu mmoja. Wao ni mmoja tu katika maana ya kuwa katika upatani. Sisi twaamini pia katika roho ya Mungu . . . Lakini hiyo si mtu kama vile roho ya maibilisi na roho ya Ulimwengu na roho ya Mpinga-Kristo isivyokuwa mtu.”—Zion’s Watch Tower, Juni 1882; Yn. 17:20-22.
-
-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kufichua Utatu
Wakiwa mashahidi wa Yehova, C. T. Russell na washirika wake walihisi sana daraka la kufichua mafundisho yaliyomwakilisha Mungu vibaya, ili kusaidia wapendao kweli wajue kwamba hayo hayakuwa na msingi wa Biblia. Wao sio waliokuwa wa kwanza kutambua kwamba Utatu si wa kimaandiko,c lakini walifahamu kwamba ikiwa wangekuwa watumishi waaminifu wa Mungu, walikuwa na daraka la kujulisha kweli juu ya utatu. Kwa ujasiri, walifunua mashina ya fundisho hilo kuu la Jumuiya ya Wakristo, kwa manufaa ya wote wapendao kweli.
Watch Tower la Juni 1882 lilitaarifu hivi: “Wanafalsafa wengi wapagani wakipata kwamba ingekuwa hekima kujiunga na orodha ya waliojiandikisha katika dini yenye kuzuka [namna fulani ya Ukristo ulioasi imani uliokubaliwa na maliki Waroma katika karne ya nne W.K.], walianza kutayarisha njia rahisi ya kuuendea kwa kujaribu kuvumbua milingano kati ya Ukristo na Upagani, na hivyo kuziunganisha zote mbili pamoja. Walifanikiwa vizuri sana. . . . Kwa kuwa ile theolojia ya kale ilikuwa na hesabu fulani ya miungu mikuu, pamoja na nusu-miungu mingi ya jinsia zote mbili, hao Wakristo-wapagani (tukiunda neno) wakaanza kutengeneza upya orodha ya theolojia hiyo mpya. Kwa hiyo, wakati huo, fundisho la Miungu watatu likabuniwa—Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu.”
Baadhi ya makasisi walijaribu kulipa fundisho lao ladha ya Kibiblia kwa kunukuu maandiko kama vile 1 Yohana 5:7, lakini Ndugu Russell alitoa uthibitisho wa kuonyesha kwamba ilijulikana sana na wasomi kwamba sehemu ya andiko hilo ilikuwa maneno yaliyoongezwa, maneno bandia yaliyopachikwa na mwandishi kuunga mkono fundisho lisilopatikana katika Maandiko. Wateteaji wengine wa Utatu walitumia Yohana 1:1, lakini Watch Tower lilichanganua andiko hilo kwa msingi wa yaliyomo na habari inayolizunguka kuonyesha kwamba hilo haliungi mkono kwa vyovyote imani katika Utatu. Kupatana na hilo, katika toleo lalo la Julai 1883, Watch Tower lilisema hivi: “Funzo zaidi la Biblia badala ya funzo la maandishi ya kanisa lingalifanya habari hiyo kuwa wazi zaidi kwa wote. Fundisho la utatu linapingana kabisa na Maandiko.”
Ndugu Russell alifichua waziwazi upumbavu wa kudai kuamini Biblia na wakati uleule kufundisha fundisho kama vile Utatu, ambalo hupingana na yale ambayo Biblia husema. Hivyo aliandika hivi: “Wanajikuta wakiwa katika mapingano yenye mvurugo kama nini wale wasemao kwamba Yesu na Baba ni Mungu mmoja! Hilo lingehusisha ndani wazo la kwamba Bwana yetu Yesu alikuwa mnafiki alipokuwa duniani na alijisingizia tu kusema na Mungu katika sala, hali Yeye Mwenyewe alikuwa Mungu yuleyule. . . . Tena, sikuzote Baba amekuwa asiyeweza kufa, kwa hiyo hangeweza kufa. Basi, Yesu angaliwezaje kufa? Mitume ni mashahidi bandia wote kwa kujulisha kifo na ufufuo wa Yesu ikiwa Yeye hakufa. Hata hivyo, Maandiko hujulisha kwamba Yeye alikufa hakika.”d
Hivyo, mapema katika historia yao ya kisasa, Mashahidi wa Yehova walikataa katakata fundisho la Utatu la Jumuiya ya Wakristo kwa kupendelea fundisho lenye kupatana na akili, lenye kuchangamsha moyo la Biblia yenyewe.e
-