-
Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi NyumbaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Adolf Weber, aliyerudi Uswisi akiwa na habari njema katika miaka ya katikati ya 1890, alikuwa na eneo kubwa lililotandaa hadi kwenye nchi kadhaa zilizohitaji kuhubiriwa. Yeye angeweza kuenezaje eneo hilo lote? Yeye binafsi alisafiri mbali akiwa kolpota, lakini pia aliweka matangazo katika magazeti ya habari na kufanya mipango ili wauza-vitabu watie ndani vichapo vya Watch Tower katika fungu lao la vitabu. Katika 1907 kikundi kidogo cha Wanafunzi wa Biblia katika Ujerumani kilipanga kwamba trakti 4,850,000 zenye kurasa nne zipelekwe kwa posta pamoja na magazeti ya habari. Punde baada ya vita ya ulimwengu ya kwanza, ndugu Mlatvia aliyekuwa mshiriki wa wafanyakazi wa makao makuu ya Sosaiti katika New York alilipia matangazo katika magazeti katika nchi alimozaliwa. Mwanamume mmoja aliyeitikia mojapo matangazo hayo alikuja kuwa Mwanafunzi wa kwanza wa Biblia katika Latvia. Hata hivyo, utumizi wa njia hizo za utangazaji haukuchukua mahali pa kutoa ushahidi kibinafsi na nyumba hadi nyumba ili kutafuta wale wanaostahili. Badala ya hivyo, ulitumiwa ili kuchochea kazi ya kupiga mbiu.
-
-
Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi NyumbaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 560]
Matangazo ya magazeti ya habari yalisaidia kufikia watu ambao hawakuwa wakifikiwa katika njia nyinginezo
-