Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mikutano Kwa Ajili ya Ibada, Funzo, na Kitia-moyo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Wakati wa sehemu kubwa ya 1923, kwenye tarehe ya kwanza ya kila mwezi, kama kichocheo cha jitihada ya umoja ya kutangaza Ufalme, nusu ya vipindi vya Sala ya usiku wa Jumatano, Mkutano wa Sifa na Ushuhuda, ilitengwa itumiwe kutoa shuhuda kuhusu utumishi wa shambani.

      Angalau kufikia 1926, mikutano ya kila mwezi ambamo utumishi wa shambani ulizungumzwa iliitwa Mikutano ya Wafanyakazi. Kwa kawaida wale walioshiriki hasa katika utumishi ndio waliohudhuria. Kwenye mikutano hiyo, njia zilizokuwa zikitumiwa kutoa ushahidi kwa wengine zilizungumzwa, na mipango ya utendaji wa wakati ujao ilifanywa. Kufikia 1928, Sosaiti ilikuwa ikihimiza makutaniko yafanye mikutano hiyo kila juma. Katika muda wa miaka mingine minne, badala ya Mikutano ya Ushuhuda (au, Julisho) Makutaniko yalikuwa yanaanza kufanya ule uliokuja kujulikana kuwa Mkutano wa Utumishi, na Sosaiti ilitia kila mtu moyo ahudhurie. Kwa zaidi ya miaka 60, makutaniko yamefanya mkutano huu wa kila juma. Kwa njia ya hotuba, mazungumzo yahusishayo ushirika wa wasikilizaji, maonyesho, na mahoji, msaada hususa umeandaliwa kuhusiana na pande zote za huduma ya Kikristo.

  • Mikutano Kwa Ajili ya Ibada, Funzo, na Kitia-moyo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kwa habari ya mazoezi katika kutoa hotuba za watu wote, katika miaka ya mapema, hilo halikufanywa kwenye mikutano ya kutaniko ya kawaida. Hata hivyo, angalau kufikia 1916, ilidokezwa kwamba wale waliohisi kwamba walikuwa na uwezekano fulani wa kuwa wasemaji wa hadhara wangeweza kuwa na darasa lao wenyewe, kukiwa labda na mzee mmoja akiwa mratibu ili kuwasikiliza na kutoa shauri kwa ajili ya kufanyia maendeleo habari inayozungumzwa na utoaji wa hotuba zao. Mikutano hiyo iliyohudhuriwa na wanaume pekee kutanikoni, baadaye ilikuja kujulikana kuwa Shule za Manabii. Alipokuwa akipitia matukio ya siku hizo, Grant Suiter alikumbuka hivi: “Uchambuzi wenye kujenga niliopata katika shule haukuwa kitu ukilinganishwa na ule niliopokea mimi binafsi kutoka kwa baba baada ya yeye kuhudhuria kimojawapo vipindi hivyo ili kunisikia nikijaribu kutoa hotuba.” Ili kusaidia wale waliokuwa wakijaribu kufanya maendeleo, ndugu walitunga na wakachapa wao wenyewe kitabu cha mafundisho cha maagizo juu ya kusema, pamoja na mihtasari ya hotuba tofauti-tofauti. Hata hivyo, baada ya wakati, hizo Shule za Manabii zilikomeshwa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki