Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unaweza Kupata Furaha Katika Familia Iliyogawanyika
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Februari 15
    • Hata wanafunzi wapya wa Biblia wanaweza kuonyesha utambuzi katika jambo hilo. Waume au wake fulani ambao si waamini huenda wasiwakataze wenzi wao wa ndoa kujifunza Biblia. Huenda hata wakakiri kwamba kufanya hivyo kunaweza kuinufaisha familia. Lakini huenda wengine wakaonyesha uadui. Esther, ambaye sasa ni Shahidi, anakiri kwamba alitenda kwa “hasira” wakati mume wake alipoanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Anasema hivi: “Nilikuwa nikitupa vitabu vyake au kuviteketeza.” Howard, ambaye mwanzoni alimpinga mke wake alipoanza kujifunza Biblia, anasema hivi: “Waume wengi wanaogopa kwamba wake zao wanadanganywa ili wajiunge na dhehebu la kidini. Huenda mume asijue jinsi ya kukabiliana na hali hiyo inayoonekana kuwa hatari na hivyo anaweza kumpinga vikali.”

      7 Mwanafunzi wa Biblia ambaye mwenzi wake wa ndoa anampinga anapaswa kusaidiwa kuona kwamba si lazima aache kujifunza Biblia. Kwa kawaida, ataweza kusuluhisha matatizo akiwa mwenye tabia-pole na kumheshimu mwenzi wake wa ndoa ambaye si mwamini. (1 Pet. 3:15) Howard anasema hivi: “Ninashukuru sana kwamba mke wangu alibaki mtulivu na hakutenda kwa hasira!” Mke wake anaeleza hivi: “Howard aliniambia kwa ukali niache kujifunza Biblia. Alisema kwamba nilikuwa nikipumbazwa akili. Badala ya kubishana naye, nilimwambia kwamba huenda anasema kweli, lakini pia nilimwambia kuwa kwa hakika sijaona wakinidanganya. Hivyo, nilimwomba asome kitabu nilichokuwa nikijifunza. Alikisoma na hakupinga mambo ambayo kilisema. Mambo hayo yalimgusa moyo sana.”

  • Unaweza Kupata Furaha Katika Familia Iliyogawanyika
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Februari 15
    • 9. Unapowahubiria kweli ya Biblia washiriki wa familia ambao si waamini, unapaswa kuzingatia tahadhari gani?

      9 Akitafakari kuhusu jinsi alivyotenda baada ya kujifunza kweli ya Biblia, Jason anasema hivi: “Nilitaka kumwambia kila mtu!” Mwanafunzi wa Biblia anapoona kwamba mambo ambayo amefundishwa kutoka katika Maandiko ni ya kweli, anaweza kufurahi sana hivi kwamba anazungumza kuhusu mambo hayo karibu kila wakati. Huenda akatarajia washiriki wa familia ambao si waamini wakubali ujumbe wa Ufalme papo hapo, lakini wanaweza kukataa habari njema. Msisimko ambao Jason alikuwa nao mwanzoni ulimwathirije mke wake? Mke wake anasema hivi: “Alinichosha sana kwa kunihubiria kila wakati.” Mwanamke fulani ambaye alikubali kweli miaka 18 baada ya mume wake kuikubali anasema hivi: “Kwanza, mimi nilihitaji kujifunza kweli hatua kwa hatua.” Ikiwa kwa sasa unajifunza Biblia na mwanafunzi ambaye mwenzi wake wa ndoa hapendi kushiriki katika ibada ya kweli, kwa nini msiwe na vipindi vya kawaida vya mazoezi ili kumsaidia mwanafunzi huyo kushughulikia mambo kwa busara? Musa alisema hivi: “Mafundisho yangu yatatiririka kama mvua, maneno yangu yatadondoka kama umande, kama mvua ya rasharasha juu ya majani.” (Kum. 32:2) Kwa kawaida, maneno machache ya kweli yanayosemwa kwa njia inayofaa na wakati unaofaa kama matone ya mvua yatakuwa na matokeo mazuri zaidi kuliko gharika ya maneno.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki