-
Jina la Mungu na Jitihada za Alfonso de Zamora za Kutokeza Maandishi SahihiMnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 1
-
-
Bila shaka, kazi iliyo muhimu zaidi kati ya kazi ambazo Zamora alifanya, ni ile ya kunakili kwa usahihi sehemu ya Biblia ambayo wengi wanaiita Agano la Kale, kutia ndani tafsiri yake ya Kilatini. Huenda alitaka hati hizo zilizosahihishwa zitumiwe sana katika kutayarisha Biblia ya Complutensian Polyglot. Mojawapo ya hati zake inapatikana katika maktaba ya El Escorial iliyo karibu na jiji la Madrid, nchini Hispania. Hati hiyo inayoitwa G-I-4, ina kitabu kizima cha Mwanzo katika Kiebrania, pamoja na tafsiri yake ya neno kwa neno katika Kilatini.
Hati hiyo ina maneno haya kwenye utangulizi wake: “Maandiko Matakatifu yanahitaji kutafsiriwa katika lugha nyingine ili mataifa yaokolewe. . . . Tumeona . . . ni jambo muhimu sana kwamba waaminifu wawe na Biblia iliyotafsiriwa neno kwa neno, yaani, kwa kila neno la Kiebrania kuwe neno lenye maana sawa katika Kilatini.” Alfonso de Zamora alikuwa na ujuzi uliohitajika kutafsiri Biblia hiyo mpya katika Kilatini kwa sababu alikuwa msomi maarufu wa lugha ya Kiebrania.
-
-
Jina la Mungu na Jitihada za Alfonso de Zamora za Kutokeza Maandishi SahihiMnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 1
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 19]
Kutafsiri Jina la Mungu
Ni muhimu kutambua jinsi Alfonso de Zamora, mwanamume msomi mwenye asili ya Kiebrania, alivyotafsiri jina la Mungu. Kama picha iliyo katika ukurasa huu inavyoonyesha, Zamora ameandika jina la Mungu kuwa “jehovah” katika maelezo yake ya pambizoni kwenye maandishi yake ya Kiebrania ya kitabu cha Mwanzo ambayo yametafsiriwa neno kwa neno katika Kilatini.
Ni wazi kuwa Zamora alikubali kutafsiriwa kwa jina hilo la Mungu kuwa “jehovah” katika Kilatini. Katika karne ya 16, wakati Biblia ilipotafsiriwa katika lugha kuu zilizotumika Ulaya, watafsiri wengi wa Biblia walitumia jina hilo jinsi lilivyokuwa katika Kilatini au likiwa limebadilishwa kidogo. Watafsiri hao wanatia ndani William Tyndale (Kiingereza, 1530), Sebastian Münster (Kilatini, 1534), Pierre-Robert Olivétan (Kifaransa, 1535) na Casiodoro de Reina (Kihispania, 1569).
Hivyo, Zamora akawa mmoja wa wasomi wa Biblia wa karne ya 16 ambao walisaidia watu kujua jina la Mungu. Jambo lililofanya watu wasilijue jina na Mungu mwanzoni ni kwamba Wayahudi waliacha kulitumia jina hilo kwa sababu za kishirikina. Kwa kufuata mapokeo hayo ya Wayahudi, watafsiri wa Biblia wa dini zinazodai kuwa za Kikristo—kwa mfano, Jerome, mtafsiri wa Vulgate ya Kilatini—waliondoa jina la Mungu na badala yake wakaweka maneno kama “Bwana”au “Mungu.”
[Picha]
Tetragramatoni ya Kiebrania iliyoongezwa ukubwa ambayo Zamora alitafsiri kuwa “yehova”
-
-
Jina la Mungu na Jitihada za Alfonso de Zamora za Kutokeza Maandishi SahihiMnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 21]
Picha iliyo kwenye ukurasa wa kwanza wa tafsiri ya Zamora ya neno kwa neno
-