-
Kimbilio la Wachapaji wa BibliaAmkeni!—2002 | Septemba 8
-
-
Iliruhusiwa, Halafu Ikapigwa Marufuku
Wakati huohuo, huko Ufaransa mteteaji maarufu wa haki za binadamu aliyekuwa Mkatoliki, Jacques Lefèvre d’Étaples, alikuwa akitafsiri Biblia katika Kifaransa akitumia Biblia ya Kilatini, ingawa pia alitumia Biblia ya Kigiriki. D’Étaples alitaka watu wa kawaida wasome Biblia. Yeye aliandika hivi: “Wakati utakuja ambapo Kristo atahubiriwa kwa njia safi bila kuchanganywa na mapokeo ya wanadamu, jambo ambalo halifanywi sasa.” Mnamo mwaka wa 1523 alichapisha tafsiri ya Kifaransa ya “Agano Jipya” huko Paris. Wanatheolojia wa Chuo Kikuu maarufu cha Sorbonne, waliipinga tafsiri hiyo kwa sababu ilikuwa katika lugha ya kienyeji. Kwa sababu ya kushambuliwa, D’Étaples alitoroka Paris na kukimbilia Strasbourg kaskazini mashariki mwa Ufaransa.
Kwa sababu ya upinzani huo, wapiga chapa nchini Ufaransa hawakuthubutu tena kuchapa Biblia za Kifaransa. Basi D’Étaples angechapa Biblia yake wapi? Antwerp ndilo jiji lililofaa. Biblia yake ya mwaka wa 1530 ilichapwa huko Antwerp na Merten de Keyser na ilikuwa tafsiri ya kwanza ya Biblia nzima ya Kifaransa. Jambo la kupendeza ni kwamba De Keyser alitoa Biblia hiyo kwa ruhusa ya Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Louvain, ambacho ni cha kale zaidi nchini Ubelgiji, na ya Maliki Mtakatifu Mroma Charles wa Tano mwenyewe! Hata hivyo, mnamo mwaka wa 1546 tafsiri ya D’Étaples iliwekwa kwenye orodha ya vitabu vilivyopigwa marufuku kwa wasomaji Wakatoliki.
-
-
Kimbilio la Wachapaji wa BibliaAmkeni!—2002 | Septemba 8
-
-
[Picha katika ukurasa wa 21]
Jacques Lefèvre d’Étaples na ukurasa unaoonyesha kichwa cha chapa yake ya Biblia ya 1530, iliyochapwa Antwerp
-