-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na ishara kubwa ilionekana katika mbingu, mwanamke amepambwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya nyayo zake, na juu ya kichwa chake palikuwa na taji la nyota kumi na mbili, na yeye alikuwa na mimba. Na yeye hupiga kilio kikuu katika uchungu mkali wake ili azae.”—Ufunuo 12:1, 2, NW.
3. Ni nini ulio utambulisho wa mwanamke anayeonwa katika mbingu?
3 Kwa mara ya kwanza Yohana aona mwanamke katika mbingu. Bila shaka, yeye si mwanamke halisi. Badala ya hivyo, yeye ni ishara, au ufananisho. (Ufunuo 1:1, NW) Yeye anafananisha nini? Katika unabii uliovuviwa, nyakati nyingine wanawake huwakilisha matengenezo ‘yaliyoolewa’ na watu mashuhuri. Katika Maandiko ya Kiebrania, Israeli walisemwa kuwa mke wa Yehova Mungu. (Yeremia 3:14) Katika Maandiko ya Kigiriki, kundi la Wakristo wapakwa-mafuta husemwa kuwa bibi-arusi wa Kristo. (Ufunuo 21:9-14) Mwanamke anayeonwa na Yohana hapa yeye pia ameolewa na mtu fulani, naye yu karibu kuzaa. Mume wake ni nani? Basi, baadaye mtoto wake ‘anadakwa mbali hadi kwa Mungu na kwenye kiti cha ufalme chake.’ (Ufunuo 12:5, NW) Hivyo kwa haki Yehova Mungu anadai mtoto ni wake. Kwa hiyo, mwanamke ambaye Yohana anaona lazima awe mke wa Yehova wa ufananisho.
4. Ni nani walio wana wa mke wa Mungu wa ufananisho, naye mtume Paulo anamwitaje huyo mwanamke anayeonwa na Yohana?
4 Zapata karne nane mapema, Yehova alikuwa amesema kwa mke huyu wa ufananisho hivi: “Wana wako wote watakuwa watu waliofundishwa na Yehova.” (Isaya 54:5, 13, NW) Yesu alinukuu unabii huu na akaonyesha kwamba wana hawa walikuwa wafuasi wake waaminifu, ambao baadaye walijumlika kuwa kundi la Wakristo wapakwa-mafuta. (Yohana 6:44, 45) Kwa hiyo washiriki wa kundi hili, wanaosemwa kuwa wana wa Mungu, ndio pia walio watoto wa mke wa ufananisho wa Mungu. (Warumi 8:14) Mtume Paulo anaongeza kibendo cha mwisho cha habari anaposema: “Yerusalemu juu ni huru, na yeye ni mama yetu.” (Wagalatia 4:26, NW) Basi, “mwanamke” anayeonwa na Yohana, ni “Yerusalemu juu.”
-
-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Pia yeye ana mimba, anavumilia maumivu ya kuzaa. Vilio vyake vya kutaka msaada wa kimungu huonyesha wakati wake wa kuzaa umekuja. Katika Biblia, mara nyingi maumivu ya kuzaa hufananisha kazi ngumu inayohitajiwa ili kutokeza tokeo la maana. (Linga Zaburi 90:2; Mithali 25:23; Isaya 66:7, 8.) Hapana shaka maumivu ya kuzaa ya aina hii yalilipata tengenezo la Yehova la kimbingu lilipojitayarishia uzawa huu wa kihistoria.
Drakoni Mkubwa wa Rangi-Moto
7. Ni ishara gani nyingine ambayo Yohana aona katika mbingu?
7 Baada ya hapo Yohana aona nini? “Na ishara nyingine ikaonekana katika mbingu, na, tazama! drakoni mkubwa wa rangi-moto, mwenye vichwa saba na pembe kumi na juu ya vichwa vyake mataji saba; na mkia wake huburuta theluthi ya nyota za mbingu, na ukazivurumisha chini kwenye dunia. Na drakoni akafuliza kusimama mbele ya mwanamke ambaye alikuwa karibu kuzaa, kwamba, wakati ambapo yeye angezaa, apate kumeza mtoto wake.”—Ufunuo 12:3, 4, NW.
8. (a) Ni nini ulio utambulisho wa huyo drakoni mkubwa wa rangi-moto? (b) Ni nini kinachoonyeshwa na drakoni huyo kuwa na vichwa saba, pembe kumi, na taji juu ya kila kichwa?
8 Drakoni huyu ni Shetani, “nyoka wa awali kabisa.” (Ufunuo 12:9; Mwanzo 3:15, NW)
-
-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Yeye anangojea mwanamke azae. Yeye anataka kumeza hiki kitoto kichanga kinachotarajiwa kwa sababu yeye anajua kwamba kinatokeza tisho baya sana katika kuendelea kuwako kwake na kule kwa ulimwengu ambao juu yao yeye anatumia utawala.—Yohana 14:30.
Mwana, wa Kiume
11. Yohana anaelezaje habari za uzawa wa huyo mtoto wa mwanamke, na ni kwa nini mtoto huitwa “mwana, wa kiume”?
11 Wakati uliowekewa mataifa kutawala bila kukatizwa na Mungu ulikuja kwenye kikomo katika 1914. (Luka 21:24) Ndipo, kwa wakati barabara, mwanamke anajifungua mtoto wake: “Na yeye akazaa mwana, wa kiume, ambaye anapaswa kuchunga mataifa yote kwa ufito wa chuma. Na mtoto wake akadakwa mbali hadi kwa Mungu na kwenye kiti cha ufalme chake. Na yule mwanamke akakimbia kwenda katika jangwa, ambako yeye ana mahali palipotayarishwa na Mungu, ili wao wapaswe kulisha yeye huko siku elfu moja mia mbili na sitini.” (Ufunuo 12:5, 6, NW) Mtoto ni “mwana, wa kiume.” Ni kwa nini Yohana anatumia usemi huu wa maradufu? Yeye anafanya hivyo kuonyesha kufaa kwa mtoto, uwezo wake wa kutawala mataifa kwa uweza wa kutosha. Unakazia pia jinsi uzawa huu ulivyo pindi ya tukio lenye maana sana, la shangwe! Una daraka la maana sana katika kuleta siri takatifu ya Mungu kwenye tamati. Kwani, mtoto huyu wa kiume hata ‘atachunga mataifa yote kwa ufito wa chuma’!
12. (a) Katika Zaburi, Yehova aliahidi nini kiunabii kwa habari za Yesu? (b) Ni nini kinachofananishwa na huyo mwanamke kuzaa mwana “ambaye anapaswa kuchunga mataifa yote kwa ufito wa chuma”?
12 Sasa, je! usemi huo unasikika kuwa wenye kuzoeleka? Ndiyo, Yehova aliahidi kiunabii kwa mintarafu ya Yesu: “Wewe utavunja wao kwa fimbo ya kifalme ya chuma, kana kwamba ni chombo cha mfinyanzi wewe utaponda wao vipande vipande.” (Zaburi 2:9, NW) Pia unabii ulitolewa kwa habari yake hivi: “Ufito wa imara yako Yehova atapeleka kutoka Sayuni, akisema: ‘Enda ukishinda katikati ya maadui wako.’” (Zaburi 110:2, NW) Kwa hiyo, uzawa ulioonwa na Yohana unahusu sana Yesu Kristo. La, si kuzaliwa kwa Yesu na bikira huko nyuma kabla ya karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu; wala haungeweza kuwa ukirejezea kuinuliwa kwa Yesu tena kwenye uhai wa roho katika 33 W.K. Zaidi ya hilo, si uhamaji. Badala ya hivyo, ni uzawa wa Ufalme wa Mungu katika 1914 ukiwa uhalisi, Yesu akiwa—sasa katika mbingu kwa karibu karne 20—ameketishwa katika kiti cha ufalme akiwa Mfalme.—Ufunuo 12:10.
13. Ni nini kinachofananishwa na huyo mtoto wa kiume ‘kudakwa mbali hadi kwa Mungu na kwenye kiti cha ufalme chake’?
13 Yehova hangeweza kamwe kuruhusu Shetani ameze mke Wake au mwana Wake aliyezaliwa hivi sasa! Wakati wa uzawa, mtoto huyo wa kiume ‘anadakwa mbali kwa Mungu na hadi kwenye kiti cha ufalme chake.’ Yeye anakuja hivyo chini ya himaya ya Yehova, ambaye ataangalia kikamili huu Ufalme uliozaliwa hivi sasa, chombo Chake cha kutakasia jina Lake takatifu.
-