Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ule Uasi-imani Mkubwa Wasitawi
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Miongoni mwa mikengeuko ya mapema kabisa kulikuwa na kutenganishwa kwa maneno “mwangalizi” (Kigiriki, e·piʹsko·pos) na “mwanamume mzee,” au “mzee” (Kigiriki, pre·sbyʹte·ros), hivi kwamba maneno hayo hayakutumiwa tena kurejezea cheo kilekile kimoja cha daraka. Mwongo mmoja hivi baada ya kifo cha mtume Yohana, Ignatius, “askofu” wa Antiokia, katika barua yake kwa Wasmirna, aliandika hivi: “Hakikisheni kwamba mwamfuata askofu [mwangalizi], kama Yesu Kristo amfuatavyo Baba, na presbiteri [baraza la wanaume wazee] kama kwamba mnafuata wale Mitume.” Hivyo Ignatius alitetea maoni ya kwamba kila kutaniko lapasa kusimamiwa na askofu mmoja,c au mwangalizi, ambaye alipaswa kutambuliwa kuwa tofauti, na mwenye mamlaka kubwa kuliko, wapresbiteri, au wanaume wazee.

  • Ule Uasi-imani Mkubwa Wasitawi
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • c Neno la Kiingereza “bishop” (askofu) hutokana na neno la Kigiriki e·piʹsko·pos (“mwangalizi”) kama ifuatavyo: kutokana na neno bisshop la Kiingereza cha Enzi ya Katikati, lililotokana na neno bisceop la Kiingereza cha Zamani, lililotokana na neno biscopus, la Kilatini cha watu wa kawaida, ambalo ni namna tofauti ya neno episcopus la Kilatini cha Baadaye, lililotokana na neno la Kigiriki e·piʹsko·pos.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki