-
Nunua Dhahabu Iliyosafishwa kwa MotoUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Lakini Walaodikia hao waliokuwa matajiri katika vitu vya kimwili ni maskini kiroho. ‘Hazina walizojiwekea mbinguni’ ni chache ikiwa wana zozote. (Mathayo 6:19-21) Wao hawakutunza jicho lao likiwa sahili, wakiupa Ufalme wa Mungu mahali pa kwanza katika maisha zao. Wao kwa kweli wamo gizani, ni vipofu, bila mwono wa kiroho. (Mathayo 6:22, 23, 33) Waaidha, yajapokuwa mavazi mazuri ambayo huenda utajiri wao wa kimwili ulinunua, machoni pa Yesu wao wako uchi. Hawana mavazi ya kiroho ya kuwatambulisha kuwa Wakristo.—Linga Ufunuo 16:15.
8. (a) Ni katika njia gani hali inayofanana na ile iliyokuwako Laodikia iko pia leo? (b) Wakristo wengine wamejidanganyaje wenyewe katika ulimwengu huu wenye pupa?
8 Ni hali yenye kugutusha kama nini! Lakini je! sisi hatuoni mara nyingi hali inayofanana na hiyo leo? Ni nini kilicho mzizi wenye kusababisha? Ni mwelekeo wa kujitumainia unaotokana na kutegemea miliki za kimwili na nyenzo za kibinadamu. Kama wale waenda-kanisani wa Jumuiya ya Wakristo, baadhi ya watu wa Yehova wamejidanganya wenyewe, wakifikiri wanaweza kumpendeza Mungu kwa kuhudhuria mikutano tu pindi kwa pindi. Wao wanajaribu kutosheka na dalili tu ya kuwa “watendaji wa neno.” (Yakobo 1:22) Yajapokuwa maonyo yenye kurudiwarudiwa kutoka jamii ya Yohana, wao wanaweka moyo wao juu ya mavazi ya mitindo-mitindo, magari, na nyumba, na juu ya maisha yenye kutegemea tafrija na anasa. (1 Timotheo 6:9, 10; 1 Yohana 2:15-17) Yote hayo yanatokeza ufahamu wa kiroho uliopumbazwa. (Waebrania 5:11, 12) Badala ya kuwa wenye uvuguvugu usiochangamsha, wanahitaji kuuwasha tena “moto wa roho” waonyeshe hamu nyingi yenye kuburudisha katika ‘kuhubiri lile neno.’—1 Wathesalonike 5:19; 2 Timotheo 4:2, 5, NW.
9. (a) Ni maneno gani ya Yesu yanayopasa kugutusha Wakristo wenye uvuguvugu, na kwa nini? (b) “Kondoo” wanaopotoka wanaweza kusaidiwaje na kundi?
9 Yesu anawaonaje Wakristo wenye uvuguvugu? Maneno yake ya unyofu yapasa yawagutushe: “Wewe hujui u mwenye taabu na mwenye kusikitikiwa na maskini na kipofu na uchi.” Dhamiri zao zimekufa ganzi kufikia hatua ya kwamba wao hata hawang’amui hali yao yenye kufadhaisha sana. (Linga Mithali 16:2; 21:2.)
-
-
Nunua Dhahabu Iliyosafishwa kwa MotoUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Imewapasa watafute ponyo kwa ajili ya upofu wao wa kiroho kwa kununua dawa ya macho yenye kuponya, si ile ya waponyaji wenyeji, bali ile ya aina ambayo ni Yesu tu awezaye kuandaa. Hiyo ingewasaidia kupata utambuzi wa kiroho, ikiwasaidia watembee katika “kile kijia cha waadilifu” na macho yao yenye kung’aa yakiwa yanalenga juu ya kufanya mapenzi ya Mungu. (Mithali 4:18, 25-27, NW)
-