Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Akawasikitikia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • Sura ya 15

      “Akawasikitikia”

      Picha katika ukurasa wa 151

      “Bwana, tunataka macho yetu yafunguliwe”

      1-3. (a) Yesu anafanya nini vipofu wawili wenye kuombaomba wanapomsihi awasaidie? (b) Neno ‘sikitikia’ linamaanisha nini? (Ona maelezo ya chini.)

      VIPOFU wawili wameketi kando ya barabara karibu sana na jiji la Yeriko. Kila siku wanakuja hapo na kutafuta mahali ambapo watu wengi wanapitia kisha wanaketi na kuanza kuombaomba. Hata hivyo, leo, watajionea jambo fulani ambalo litabadili kabisa maisha yao.

      2 Kwa ghafula, waombaji hao wanasikia makelele. Kwa kuwa hawawezi kuona kinachoendelea, mmoja wao anauliza makelele hayo ni ya nini, naye anaambiwa: “Yesu Mnazareti anapitia hapa!” Yesu anaelekea Yerusalemu kwa mara ya mwisho. Hata hivyo, hayuko peke yake; umati mkubwa unamfuata. Baada ya kuambiwa ni nani anayepitia hapo, waombaji hao wanapaaza sauti na kusema: “Bwana, uturehemu, Mwana wa Daudi!” Umati unakasirika na kuwaambia waombaji hao wanyamaze, lakini watu hao wanahitaji sana msaada. Hawakubali kunyamazishwa.

      3 Ingawa kuna makelele ya umati, Yesu anawasikia waombaji hao wakipaaza sauti. Atafanya nini? Ana mambo mengi akilini na moyoni. Juma la mwisho la maisha yake duniani linakaribia. Anajua atateswa na kuuawa kikatili Yerusalemu. Hata hivyo, hapuuzi vilio vyao vya kusihi. Anasimama na kuagiza kwamba waombaji hao waletwe kwake. Waombaji hao wanamsihi: “Bwana, tunataka macho yetu yafunguliwe.” Yesu ‘anawasikitikia,’ kisha anayagusa macho yao, nao wanaanza kuona tena.a Papo hapo, wanaanza kumfuata Yesu.—Luka 18:35-43; Mathayo 20:29-34.

  • “Akawasikitikia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki