Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Utapata Baraka za Yehova?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Septemba 15
    • Boazi Alimsikiliza Mungu

      10. Boazi na Nabali walifanana katika mambo gani?

      10 Ingawa Boazi na Nabali hawakuishi wakati mmoja, kuna mambo fulani yanayofanana katika maisha yao. Kwa mfano, wanaume hao wawili waliishi katika nchi ya Yuda. Walikuwa wamilikaji-ardhi matajiri, na wote wawili walikuwa na fursa ya pekee ya kumwonyesha upendo-fadhili mtu fulani mwenye uhitaji. Lakini walifanana katika mambo hayo tu.

      11. Boazi alionyeshaje kwamba aliendelea kumsikiliza Yehova?

      11 Boazi aliishi katika kipindi cha waamuzi wa Israeli. Aliwatendea wengine kwa heshima, nao wavunaji wake walimstahi sana. (Ruthu 2:4) Alitii Sheria kwa kuhakikisha kwamba masazo ya mavuno yaliachwa shambani mwake kwa ajili ya wenye shida na maskini. (Mambo ya Walawi 19:9, 10) Boazi alifanya nini alipopata habari kuhusu Ruthu na Naomi na kuona bidii ya Ruthu ya kumruzuku mama-mkwe wake mzee? Alimjali sana Ruthu, akaamuru watumishi wake wamruhusu aokote masazo kwenye shamba lake. Kwa maneno na matendo yake ya upendo, Boazi alionyesha kwamba alikuwa mtu wa kiroho aliyemsikiliza Yehova. Kwa hiyo, alipata kibali na baraka za Mungu.—Mambo ya Walawi 19:18; Ruthu 2:5-16.

      12, 13. (a) Boazi alionyeshaje staha kubwa kwa sheria ya Yehova ya ukombozi? (b) Boazi alipata baraka gani kutoka kwa Mungu?

      12 Uthibitisho wenye kutokeza kwamba Boazi aliendelea kumsikiliza Yehova ni jinsi alivyofuata sheria ya Mungu ya ukombozi. Boazi alifanya yote awezayo kuhakikisha kwamba urithi wa mtu wa jamaa yake—Elimeleki, mume aliyekufa wa Naomi—ungebaki katika familia yake. Kupitia “mpango wa ndoa ya ndugu-mkwe,” mjane angepaswa kuolewa na mtu wa jamaa wa karibu ili mwana wanayezaa aweze kuhifadhi urithi. (Kumbukumbu la Torati 25:5-10, NW; Mambo ya Walawi 25:47-49) Ruthu alijitoa aolewe badala ya Naomi, ambaye alikuwa amepita umri wa kuzaa. Baada ya mtu wa jamaa ya karibu ya Elimeleki kukataa kumsaidia Naomi, Boazi alimwoa Ruthu. Mwana wao Obedi alionwa kuwa uzao wa Naomi na mrithi halali wa Elimeleki.—Ruthu 2:19, 20; 4:1, 6, 9, 13-16.

      13 Boazi alipata baraka nyingi kwa sababu ya kufuata sheria ya Mungu bila ubinafsi. Kupitia mwana wao Obedi, Boazi na Ruthu walipata pendeleo la kuwa babu na nyanya wa Yesu Kristo. (Ruthu 2:12; 4:13, 21, 22; Mathayo 1:1, 5, 6) Kutokana na matendo ya Boazi yasiyokuwa na ubinafsi, tunajifunza kwamba wale wanaowapenda wengine na kufuata matakwa ya Mungu hupata baraka.

  • Je, Utapata Baraka za Yehova?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Septemba 15
    • 16. Tunawezaje kumwiga Boazi na kukataa njia za Nabali?

      16 Boazi na Nabali walitofautiana kama nini! Acheni tuige fadhili na ukarimu wa Boazi na kukataa njia za ukatili na ubinafsi za Nabali. (Waebrania 13:16) Tunaweza kufanya hivyo kwa kutumia ushauri huu wa mtume Paulo: “Maadamu tuna wakati wenye kufaa kwa ajili ya hilo, acheni sisi tufanye lililo jema kuelekea wote, lakini hasa kuelekea wale ambao katika imani ni jamaa zetu.” (Wagalatia 6:10) Leo “kondoo wengine” wa Yesu, ambao ni Wakristo walio na tumaini la kuishi duniani, wana pendeleo la kuwafanyia mema watiwa-mafuta wa Mungu, mabaki ya wale 144,000, ambao watapewa uhai usioweza kufa mbinguni. (Yohana 10:16; 1 Wakorintho 15:50-53; Ufunuo 14:1, 4) Yesu huona matendo hayo ya upendo kana kwamba anatendewa yeye binafsi, na kufanya mambo hayo huleta baraka nyingi za Yehova.—Mathayo 25:34-40; 1 Yohana 3:18.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki