-
Hekalu Kubwa la Kiroho la YehovaMnara wa Mlinzi—1996 | Julai 1
-
-
9. (a) Pazia kati ya Patakatifu na Patakatifu Zaidi Sana lilifananisha nini? (b) Yesu aliingiaje ndani kupita lile pazia la hekalu la kiroho la Mungu?
9 Lile pazia lililotenganisha Patakatifu na Patakatifu Zaidi Sana lilifananisha mwili wa Yesu wenye nyama. (Waebrania 10:19, 20) Lilikuwa kizuizi kilichomzuia Yesu asiingie mbele ya Babaye alipokuwa mwanadamu duniani. (1 Wakorintho 15:50) Wakati wa kifo cha Yesu, ‘pazia la hekalu lilipasuka vipande viwili toka juu hata chini.’ (Mathayo 27:51) Hilo lilionyesha kwa njia yenye kutokeza kwamba kizuizi kilichomzuia Yesu asiingie mbinguni sasa kilikuwa kimeondolewa. Siku tatu baadaye, Yehova Mungu alifanya muujiza wenye kutokeza. Alimfufua Yesu kutoka kwa wafu, si akiwa mwanadamu awezaye kufa mwenye nyama na damu, bali akiwa kiumbe kitukufu cha kiroho, ‘akaaye milele.’ (Waebrania 7:24) Siku arobaini baadaye, Yesu alipaa kwenda mbinguni akaingia “Patakatifu pa Patakatifu” (NW) palipo halisi, “aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu.”—Waebrania 9:24.
-
-
Hekalu Kubwa la Kiroho la YehovaMnara wa Mlinzi—1996 | Julai 1
-
-
3. (a) Yesu alimaanisha nini kwa maneno, “Dhabihu na toleo hukutaka”? (b) Ni kielelezo gani chenye kutokeza alichoweka Yesu kwa wote wanaotaka kuwa wanafunzi wake?
3 Wakati wa ubatizo wake Yesu alikuwa akisali. (Luka 3:21) Kwa hakika, kuanzia wakati huo maishani mwake na kuendelea, alitimiza maneno ya Zaburi 40:6-8, kama ionyeshwavyo baadaye na mtume Paulo: “Dhabihu na toleo hukutaka, lakini mwili uliniwekea tayari.” (Waebrania 10:5) Kwa njia hiyo Yesu alionyesha kujua kwake kwamba Mungu ‘hakutaka’ dhabihu za wanyama ziendelee kutolewa kwenye hekalu la Yerusalemu. Badala ya hilo, alitambua kwamba Mungu alikuwa amemtayarishia yeye, Yesu, mwili mkamilifu wa kibinadamu, apate kuutoa ukiwa dhabihu. Hilo lingeondoa uhitaji wowote zaidi wa dhabihu za wanyama. Akionyesha tamaa yake yenye kuhisiwa moyoni ya kunyenyekea mapenzi ya Mungu, Yesu aliendelea kusali: “Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) niyafanye mapenzi yako, Mungu.” (Waebrania 10:7) Ni kielelezo kitukufu kama nini cha moyo mkuu na ujitoaji usio na ubinafsi alichoweka Yesu siku hiyo kwa wote ambao baadaye wangekuwa wanafunzi wake!—Marko 8:34.
4. Mungu alionyeshaje kukubali kwake kule kujitoa mwenyewe kwa Yesu?
4 Je, Mungu alionyesha kukubali sala ya Yesu ya ubatizo? Acheni mmoja wa mitume wateule wa Yesu atupe jibu: “Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua akija juu yake; na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye.”—Mathayo 3:16, 17; Luka 3:21, 22.
5. Ni nini kilichofananishwa na madhabahu halisi ya hekalu?
5 Kukubali kwa Mungu kule kutolewa kwa mwili wa Yesu utumiwe ukiwa dhabihu kulimaanisha kwamba, katika maana ya kiroho, madhabahu iliyo kubwa zaidi ya ile iliyokuwa katika hekalu la Yerusalemu ilichukua sehemu ya kwanza. Madhabahu halisi ambapo wanyama walitolewa kwa ajili ya dhabihu ilitangulia kuonyesha madhabahu hiyo ya kiroho, ambayo kwa kweli ilikuwa “mapenzi” au mpango wa Mungu wa kukubali uhai wa Yesu wa kibinadamu ukiwa dhabihu. (Waebrania 10:10) Hiyo ndiyo sababu mtume Paulo aliweza kuwaandikia Wakristo wenzake: “Tuna madhabahu ambayo wale waihudumiao ile hema hawana ruhusa kula vitu vyake.” (Waebrania 13:10) Kwa maneno mengine, Wakristo wa kweli hufaidika kutokana na dhabihu ya kufunika dhambi iliyo bora zaidi, ambayo makuhani Wayahudi walio wengi walikataa.
-