Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tembea Kupatana na Roho ili Upate Uzima na Amani
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Novemba 15
    • Mwili wetu wenye dhambi unatuchochea sikuzote kufanya mambo yasiyompendeza Mungu, lakini mambo hayo yanaongoza tu kwenye kifo. Katika barua yake kwa Wagalatia, Paulo aliyaita matendo na tabia kama hizo kuwa “matendo ya mwili.” Kisha akaongeza hivi: “Wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Gal. 5:19-21) Watu wa aina hiyo ni sawa na wale wanaotembea kupatana na mwili. (Rom. 8:4) ‘Mambo yanayowaongoza’ na ‘viwango wanavyofuata maishani’ ni vya kimwili kabisa. Je, ni wale tu ambao wanafanya uasherati, kuabudu sanamu, kuwasiliana na pepo, au kutenda dhambi nyingine nzito ndio wanaotembea kupatana na mwili? Hapana, kwa kuwa matendo ya mwili yanatia ndani pia mambo ambayo huenda wengine wakayaona kuwa tu kasoro za utu, kama vile wivu, milipuko ya hasira, ugomvi, na kuwaonea wengine kijicho. Ni nani anayeweza kusema kwamba yeye ameacha kabisa kutembea kupatana na mwili?

  • Tembea Kupatana na Roho ili Upate Uzima na Amani
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Novemba 15
    • 14. Wale wanaoishi ‘kupatana na mwili’ wana mwelekeo gani?

      14 Katika barua hiyohiyo kwa Waroma, Paulo alizungumza kuhusu aina mbili za watu ambao wanakaza akili juu ya mambo mawili yanayotofautiana kabisa. (Soma Waroma 8:5.) Hapa neno “mwili” halimaanishi tu mwili halisi. Katika Biblia, neno “mwili” nyakati nyingine linatumiwa kumaanisha hali ya dhambi na kutokamilika kwa mwili wetu. Hali hiyo ndiyo inayosababisha pambano kati ya mwili na akili, pambano ambalo Paulo alitaja awali. Hata hivyo, tofauti na Paulo, wale wanaoishi ‘kupatana na mwili’ hawajaribu hata kidogo kupambana na tamaa zao mbaya. Badala ya kuchunguza yale ambayo Mungu anataka wafanye na kukubali msaada ambao ameandaa, watu hao wana mwelekeo wa ‘kukaza akili zao juu ya mambo ya mwili.’ Mara nyingi wanakaza akili zao juu ya kutosheleza tamaa zao za mwili na kuponda raha. Kinyume na hilo, wale wanaoishi ‘kupatana na roho’ wana mwelekeo wa kukaza akili zao juu ya “mambo ya roho,” yaani, maandalizi na utendaji wa kiroho.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki