-
Kutokeza Fasihi za Biblia Ili Zitumiwe Katika HudumaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kujapokuwa na upinzani mwingi kwa kazi yetu huko, Sosaiti ilianzisha kiwanda cha kuchapa katika Cluj, ili kupunguza gharama za fasihi na kuifanya ipatikane kwa urahisi zaidi kwa watu wenye njaa ya kweli katika Rumania na nchi zilizo karibu. Katika 1924 kiwanda hicho kiliweza kutokeza vitabu vilivyojalidiwa karibu robo milioni, kwa kuongezea magazeti na vijitabu, katika Kirumania na Kihungaria.
-
-
Kutokeza Fasihi za Biblia Ili Zitumiwe Katika HudumaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katika Ujerumani kufuatia Vita ya Ulimwengu 1, idadi kubwa ya watu walikuwa wakimiminika kwenye mikutano ya Wanafunzi wa Biblia. Lakini Wajerumani walikuwa wakipata taabu kubwa ya kiuchumi. Ili kupunguza gharama ya fasihi za Biblia kwa manufaa yao, Sosaiti ilisitawisha kazi ya uchapaji yayo yenyewe huko pia. Katika Barmen, mwaka 1922, uchapaji ulifanywa kwa kutumia matbaa-tambarare kwenye sehemu ya ngazi katika Kao la Betheli na kwenye nyingine katika kibanda cha mbao. Mwaka uliofuata akina ndugu walihamia Magdeburg kwenye vifaa bora zaidi. Walikuwa na majengo mazuri huko, mengine yaliongezwa, na vifaa vya kuchapa na kujalidi vitabu vikawekwa. Kufikia mwisho wa 1925, iliripotiwa kwamba uwezo wa kutokeza vitabu wa kiwanda hicho ungekuwa mkubwa angalau kama ule uliotumiwa kwenye makao makuu katika Brooklyn.
-