Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matangazo
    Huduma ya Ufalme—2007 | Novemba
    • Matangazo

      ◼ Toleo la Novemba: Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mwenye nyumba akisema hana watoto, mtolee broshua Endeleeni Kukesha! Desemba: Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Au unaweza kutoa kitabu Mkaribie Yehova au Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 ambacho kina karatasi zinazobadilika rangi, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1991. Makutaniko ambayo hayana vitabu hivyo yanaweza kutoa kitabu Ujuzi au broshua Endeleeni Kukesha! Februari: Kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia au kitabu Ujuzi.

      ◼ Kwa kuwa Desemba ina Jumamosi na Jumapili tano, utakuwa ni mwezi mzuri wa kufanya upainia msaidizi.

      ◼ Kuna vichapo kadhaa ambavyo vimekusudiwa kuwafikia watu wa utamaduni na dini mbalimbali. Mtumishi wa vitabu ana orodha ya vichapo hivyo muhimu.

      ◼ Hundi zinazotolewa kama michango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote katika makusanyiko ya wilaya na zile zinazotumwa kwenye ofisi ya tawi ziandikwe jina la shirika linalotambuliwa kisheria katika nchi yenu.

      ◼ Wahubiri wote wanahimizwa wajaze kadi ya mamlaka ya kudumu ya uwakilishi (DPA) au kadi ya mwelekezo wa mapema kuhusu tiba/ondoleo la hatia (AMD), ikiwa hawajafanya hivyo. Kadi hiyo ya DPA inalinda haki yako ya kukataa kutiwa damu. Wazee watatoa msaada kwa mtu mmoja-mmoja kulingana na uhitaji.—Ona nyongeza katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 2006.

      ◼ Wahubiri hawahitaji tena kujaza fomu ya Ripoti ya Funzo (S-3) kwa ajili ya kila funzo la Biblia lililoongozwa katika mwezi. Hata hivyo, wanapaswa kuendelea kuonyesha idadi ya mafunzo yaliyoongozwa kwenye safu inayofaa katika fomu ya Ripoti ya Utumishi wa Shambani (S-4). Bila kukawia, fomu ya S-3 itumiwe tu kuandika hudhurio la mikutano.

  • Sanduku la Swali
    Huduma ya Ufalme—2007 | Novemba
    • Sanduku la Swali

      ◼ Je, ni sawa kuandika anwani yetu ya barua-pepe katika vichapo tunavyowaachia watu?

      Wahubiri fulani huweka muhuri au vibandiko vyenye anwani yao ya barua-pepe kwenye magazeti au trakti ambazo wanawaachia watu. Watu ambao wanapokea vichapo hivyo wanaweza kuwasiliana na wahubiri hao ikiwa wanataka habari zaidi. Jitihada hizo za kuwasaidia watu ambao wanapendezwa zinafanywa kwa nia nzuri. Hata hivyo, kituo chetu rasmi cha Intaneti tayari kimeonyeshwa kwenye ukurasa wa nyuma wa magazeti na trakti. Kwa hiyo, haingefaa tuandike anwani yetu ya barua-pepe katika vichapo.

      Mhubiri mwenyewe ataamua ikiwa atawapa watu katika eneo anwani yake ambayo ameandika kwenye karatasi, hasa anapofanya ziara za kurudia. Tunapaswa kuwarudia wale wanaopendezwa badala ya kungojea wawasiliane nasi ikiwa wanataka habari zaidi. Tutajua ikiwa mtu anapendezwa kikweli kwa kuzungumza naye uso kwa uso.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki