-
Barua Kutoka Ofisi ya TawiHuduma ya Ufalme—2006 | Septemba
-
-
Barua Kutoka Ofisi ya Tawi
Wahubiri wa Ufalme Wapendwa:
Tungependa kuwashukuru kwa msaada wenye upendo ambao mliwatolea ndugu na dada wengi walioathiriwa na ukame na mafuriko ambayo yalisababisha upungufu wa chakula katika wilaya fulani kwenye eneo letu.—Yoh. 13:35.
Ndugu mmoja aliyepokea msaada wa chakula alisema: “Msaada ulikuja kwa wakati uliofaa kabisa. Tunamshukuru sana Yehova na tengenezo lake kwa msaada huu. Tumeshuhudia upendo halisi unaotambulisha Wakristo wa kweli.” Michango yenu kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote inathaminiwa sana.
Kwa mfano, huko Marekani maelfu ya ndugu na dada walipokea msaada wenye upendo walipoathiriwa na tufani zilizoharibu eneo la Ghuba ya Pwani mwaka wa 2005. Zaidi ya ndugu na dada 8,000 waliokuwa wakifanya kazi chini ya Halmashauri za Ujenzi za Mkoa zipatazo 60 walitoa muda wao, ujuzi, na mali zao ili kuwasaidia wengine. Walirekebisha na kujenga upya Majumba ya Ufalme 86 na nyumba 4,178. Ili waweze kusaidia, baadhi ya akina ndugu walisafiri kutoka maeneo yote ya nchi ya Marekani. Tunathamini kama nini jitihada zao za upendo!—1 The. 5:18.
Mjitoleaji mmoja kutoka Michigan alisema: “Nilifurahi sana kuona tabasamu za familia mbalimbali walipoona paa mpya tulizoezeka kwenye nyumba zao. Siwezi kueleza jinsi ninavyohisi kuwa sehemu ya undugu huu wa ajabu.” Kwa kweli huo ni mfano mzuri wa jinsi ya kuwasaidia wale waliokumbwa na janga hilo.
Tunaomba mwendelee kusali kwa ajili ya ndugu zetu wapendwa ambao huenda wameathiriwa na majanga mengi yanayotokea siku hizi za mwisho na vilevile kwa ajili ya wanaotoa msaada.—2 Kor. 1:11.
Ndugu zenu,
Ofisi ya Tawi ya Burundi, Kenya, Sudan, Tanzania, na Uganda
-
-
Kampeni ya Pekee Oktoba 16–Novemba 12!Huduma ya Ufalme—2006 | Septemba
-
-
Kampeni ya Pekee
Oktoba 16–Novemba 12!
1 “Mwisho wa Dini ya Uwongo Unakaribia!” Hicho ndicho kichwa cha trakti Habari za Ufalme Na. 37, ambayo itagawanywa ulimwenguni pote kuanzia mwezi ujao. Nusu ya kwanza ya Oktoba, tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kuanzia Jumatatu Oktoba 16, hadi Jumapili, Novemba 12, tutashiriki katika kazi kubwa ya kugawanya trakti Habari za Ufalme Na. 37. Kwenye miisho ya juma ya kampeni hiyo, tutaitoa pamoja na magazeti ya karibuni.
2 Nani Wanaweza Kushiriki?: Wote ambao hushiriki kuhubiri habari njema watapenda kufanya hivyo kwa ukamili. Wengine wataweza kuwa mapainia-wasaidizi. Je, una watoto au mafunzo ya Biblia ambayo yanafanya maendeleo ya kiroho? Wasaidie wawaendee wazee ili waone ikiwa wanastahili kuwa wahubiri ambao hawajabatizwa. Wazee wanapaswa kuchukua hatua ya kuzungumza na wahubiri wasiotenda na kuwatia moyo washiriki, labda wakihubiri pamoja na wahubiri wenye uzoefu.
3 Makutaniko yote yatatumiwa trakti Habari za Ufalme Na. 37 ili wahubiri na mapainia waweze kupata nakala 50 hivi. Watu wanaopendezwa ambao bado hawajaanza kuhubiri wanaweza kupata nakala tano ili wawagawie washiriki wa familia na marafiki. Wahubiri wanapaswa kuweka rekodi ya trakti watakazotoa na kuandika idadi hiyo nyuma ya ripoti ya utumishi wa shambani mwishoni mwa Oktoba na Novemba. Mwandishi atahesabu trakti ambazo kutaniko lote lilitoa na kuripoti kwa ofisi ya tawi mwishoni mwa kila mwezi. Nakala zozote za trakti Habari za Ufalme zinazosalia baada ya kampeni hiyo kwisha zinaweza kutumiwa katika sehemu yoyote ya huduma.
4 Mambo ya Kusema: Zungumza kwa ufupi ili uweze kugawa ujumbe huo katika eneo kubwa. Unaweza kusema hivi: “Ninashiriki katika kazi inayofanywa ulimwenguni pote ya kugawa ujumbe huu muhimu kwa manufaa ya watu wote. Hii ni nakala yako. Tafadhali isome.” Katika maeneo fulani huenda ikafaa zaidi kutobeba mfuko unapoenda nyumba kwa nyumba. Hakikisha kwamba unaweka rekodi sahihi kila mahali unapopata upendezi.
5 Jinsi ya Kushughulikia Eneo Lenu: Badala ya kugawa trakti ya Habari za Ufalme barabarani, kazieni hasa eneo lenu la nyumba kwa nyumba na la biashara. Andika vizuri nyumba ambamo watu hawapatikani, na ujaribu kurudi wakati mwingine au siku nyingine ya juma. Kuanzia Jumatatu, Novemba 6, unaweza kuacha nakala moja ya trakti hiyo kwenye nyumba ambamo watu hawapatikani. Hata hivyo, iwapo kutaniko lina eneo kubwa sana hivi kwamba lote halitaweza kukamilishwa kwa wakati uliowekwa, wazee wanaweza kuamua iwapo trakti Habari za Ufalme inaweza kuachwa kwenye nyumba ambamo watu hawapatikani wakati wa kampeni yote.
6 Kuharibiwa kwa “Babiloni Mkubwa” kunakaribia haraka. Watu wanahitaji kutoka kwake kabla haijaharibiwa. (Ufu. 14:8; 18:8) Fanya mipango sasa ili ushiriki kikamili katika kampeni hii ya ulimwenguni pote ya kuwajulisha watu wote kwamba mwisho wa dini ya uwongo unakaribia!
-