-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Agosti 1941 barua zote zilizotumwa na ofisi ya tawi zilitwaliwa na wenye mamlaka waliokuwa wameweka vikwazo, nasi hatukupewa sababu yoyote. Baadaye, mwaka huohuo, waziri wa mambo ya ndani alitoa amri vichapo vyote vya tengenezo vilivyo nchini vitwaliwe. Saa nne asubuhi moja, maofisa wa Idara ya Upelelezi (CID) walifika kwenye ofisi ya tawi wakiwa na malori ili kuchukua vichapo vyote. Ndugu Phillips aliichunguza hati ya kukamata, akaona kwamba haikupatana kikamili na sheria. Vitabu havikuorodheshwa kulingana na jina, kama ilivyopaswa kuwa kulingana na Gazeti la Serikali.
Kisha Ndugu Phillips akawaomba maofisa wa CID wasubiri awasiliane na wakili, naye akatoa ombi la haraka kwa mahakama kuu itoe amri ya kumzuia waziri wa mambo ya ndani asitwae vichapo hivyo. Ombi lake likakubaliwa. Kufikia alasiri amri hiyo ilitolewa, nao polisi wakaondoka mikono mitupu. Siku tano baadaye waziri huyo alifutilia mbali amri hiyo na kulipia gharama zetu za kisheria.
-
-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 84]
Familia ya Betheli huko Cape Town mwaka wa 1931, kutia ndani George na Stella Phillips
[Picha katika ukurasa wa 87]
Kunasa sauti katika Kihosa
[Picha katika ukurasa wa 87]
Andrew Jack na mashini ya kuchapisha inayoitwa Frontex, 1937
-