-
Matukio Muhimu ya mwaka uliopita2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
OFISI ZA TAWI ZAWEKWA WAKFU
Kulikuwa na shangwe kubwa kwenye ofisi ya tawi ya Afrika Kusini Jumamosi (Siku ya Posho), Novemba 10, 2007, wakati ndugu na dada 4,000 hivi walipokusanyika kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa kiwanda cha uchapishaji kilichopanuliwa, chumba cha kulia chakula, na jengo la makao.
Waliotembelea kiwanda hicho walifurahia kuona mashini za uchapaji zinazoitwa MAN Roland Lithoman zikichapisha makumi ya maelfu ya Biblia na vichapo vya Biblia. Mashini mpya ya kujalidi vitabu tayari imejalidi nakala zaidi ya milioni moja za Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika lugha 16 za Afrika. Wageni walionyeshwa jengo la idara ya upakizi na usafirishaji lililopanuliwa ambapo ofisi inaweka vichapo vya Biblia vinavyotumiwa na makutaniko 8,000 hivi katika nchi kumi kusini mwa Afrika.
-
-
Matukio Muhimu ya mwaka uliopita2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 29]
Kiwanda cha uchapishaji, ofisi ya tawi ya Afrika Kusini
-