-
Kutokeza Fasihi za Biblia Ili Zitumiwe Katika HudumaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kufikia mwisho wa 1975, Watch Tower Society ilikuwa ikichapa fasihi za Biblia katika vifaa vyayo yenyewe katika nchi 23 duniani pote—vitabu katika nchi tatu; vijitabu au magazeti au yote mawili katika sehemu zote 23. Sosaiti ilikuwa ikitokeza tena vitu vidogovidogo zaidi katika vifaa vyayo yenyewe, katika nchi 25.
-
-
Kutokeza Fasihi za Biblia Ili Zitumiwe Katika HudumaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kufikia 1992 Watch Tower Society ilikuwa na jumla ya vifaa vya kujalidi 28 vikiendeshwa katika nchi nane tofauti.
Katika mwaka uo huo, 1992, si kwamba tu Watch Tower Society ilikuwa ikichapa fasihi za Biblia katika lugha 180 katika Marekani bali pia viwanda vyayo vikubwa vinne vya kuchapia katika Amerika ya Latin vilikuwa vikiandaa fasihi nyingi zilizohitajiwa nchini humo na pia katika nchi nyinginezo katika sehemu hiyo ya ulimwengu. Viwanda vingine 11 vilikuwa vikitokeza fasihi katika Ulaya, na zote hizo zilikuwa zinasaidia kujazia uhitaji wa fasihi wa nchi nyinginezo. Kati ya hizo, Ufaransa ilikuwa ikitoa fasihi kwa nchi 14, na Ujerumani, ambayo ilichapa katika lugha zaidi ya 40, ilikuwa ikisafirisha ugavi mkubwa kwa nchi 20 na ugavi mdogo zaidi kwenye nchi nyinginezo nyingi. Barani Afrika, viwanda sita vya kuchapia vya Watch Tower vilikuwa vikitokeza fasihi za Biblia katika jumla ya lugha 46. Viwanda vingine 11 vya kuchapia—vingine vikubwa, vingine vidogo—vilikuwa vikiandalia Mashariki ya Kati na Mashariki ya Mbali, visiwa vya Pasifiki, Kanada, na maeneo mengineyo fasihi za kutumia katika kueneza ujumbe wenye uharaka kuhusu Ufalme wa Mungu. Katika nchi 27 nyingine, Sosaiti ilikuwa ikichapa vitu vidogovidogo vilivyohitajiwa na makutaniko ili yatende kazi vema.
-