-
Kutegemezwa na Uhakika Wangu Katika YehovaMnara wa Mlinzi—1997 | Februari 1
-
-
Katika Julai 1, 1949, nilisisimuka kualikwa kutumikia Betheli, kama vile ofisi za tawi za Mashahidi wa Yehova katika nchi fulani-fulani ziitwavyo. Siku hizo Betheli katika Brazili ilikuwa kwenye 330 Licínio Cardoso Street katika Rio de Janeiro.
-
-
Kutegemezwa na Uhakika Wangu Katika YehovaMnara wa Mlinzi—1997 | Februari 1
-
-
Majengo Yetu ya Betheli
Limekuwa jambo la kusisimua katika miaka ambayo imepita kuona upanuzi wa majengo yetu ya Betheli Brazili. Katika mwaka wa 1952 tulijenga kiwanda chenye orofa mbili nyuma ya makao yetu ya Betheli katika Rio de Janeiro. Kisha katika 1968, Betheli ilihamishwa hadi jengo jipya katika jiji la São Paulo. Tulipohamia huko, kila kitu kilionekana kikubwa na chenye nafasi kwa familia yetu ya Betheli yenye washiriki 42. Kwa kweli tulifikiria kwamba jengo hilo lingetosha kwa ukuzi wetu wote wa wakati ujao. Hata hivyo, katika mwaka wa 1971 maongezeo mawili yenye orofa tano yalijengwa, na kiwanda kilichokuwa karibu kikanunuliwa, kikajengwa upya, na kuunganishwa na majengo hayo. Lakini baada ya miaka michache, ongezeko lenye kuendelea la wapiga-mbiu wa Ufalme—tulipita alama ya 100,000 katika mwaka wa 1975—lilihitaji nafasi zaidi.
Kwa hivyo, majengo mapya yalijengwa karibu kilometa 140 kutoka São Paulo karibu na mji mdogo wa Cesário Lange. Katika mwaka wa 1980 familia yetu ya Betheli yenye washiriki 170 ilihamishwa kwenda kwenye majengo hayo mapya. Tangu wakati huo kazi ya Ufalme imekua kwa njia ya kutazamisha. Sasa tuko na watu zaidi ya 410,000 wanaoshiriki kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri Brazili! Kushughulikia mahitaji ya kiroho ya wapiga-mbiu hawa wote wa Ufalme, tumelazimika kuendelea kujenga viwanda vipya vya kuchapia fasihi za Biblia na makao mapya ili kuwapa malazi wajitoleaji wa Betheli. Sasa tuna washiriki wapatao 1,100 wa familia ya Betheli!
-