-
Matukio Muhimu Ya Mwaka Uliopita2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ofisi ya Tawi ya Ufilipino Yawekwa Wakfu
“Tunataka kazi yetu ya ujenzi iwe nzuri kama ya Watch Tower!” Hivyo ndivyo wajenzi fulani ambao si Mashahidi walivyosema huko Manila baada ya kuona jinsi ofisi ya tawi ya Ufilipino ilivyojengwa kwa ustadi. Wapiga picha wa televisheni waliokuwa wakitayarisha kipindi fulani kuhusu sheria za ujenzi walimtembelea injinia mmoja wa jiji, naye akawaambia hivi: “Ikiwa mnataka kuwaona watu wanaofuata sheria za ujenzi kwa makini, nendeni kwenye Watch Tower.”
Mbali na jengo jipya la makao lenye orofa kumi, ndugu walijenga nyumba nyingine za ziada na kurekebisha jengo la makao lenye orofa kumi lililojengwa mwaka wa 1991. Kwa nini upanuzi huo ulihitajiwa? Kuanzia mwaka wa 1991 hadi 2003 idadi ya wahubiri iliongezeka kwa wahubiri 34,000 na kukawa na kilele kipya cha wahubiri wa Ufalme zaidi ya 144,000!
Ofisi hiyo iliwekwa wakfu Novemba 1, 2003. Wanabetheli, wamishonari waliokuwa huko zamani, wageni kutoka nchi 13, na ndugu na dada wenyeji zaidi ya 2,000 walihudhuria Jumamosi asubuhi. Wote walikuwa 2,540. Stephen Lett alitoa hotuba yenye kichwa, “Kuthamini Nyumba za Ibada za Yehova za Kale na za Wakati Huu.” Siku iliyofuata, mapainia na wazee wa makutaniko pamoja na wake zao walifurahia programu ya pekee kwenye Jumba la Kusanyiko la Metro Manila. Wote walikuwa 8,151.
-
-
Matukio Muhimu Ya Mwaka Uliopita2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 30]
Ofisi ya tawi ya Ufilipino iliyopanuliwa
-