-
Matukio Muhimu Ya Mwaka Uliopita2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ofisi ya Tawi ya India Yawekwa Wakfu
Ofisi ya tawi ya India inaandika: “Hatimaye siku iliyongojewa kwa muda mrefu ilifika Desemba 7, 2003. Hiyo ilikuwa siku ya kuwekwa wakfu kwa ofisi yetu iliyojengwa karibuni huko Bangalore. Jiji hilo liko kwenye eneo la katikati, kusini mwa India.”
Ofisi hiyo yenye ukubwa wa meta 30,000 za mraba, iliyojengwa kwenye kiwanja chenye ukubwa wa ekari 43, ni kama mji mdogo. Hiyo ni ofisi ya tawi ya kwanza ulimwenguni kujengwa na kampuni ya ujenzi, nayo ina mtambo wa kusafishia maji ya kunywa, mtambo wa kusafishia maji machafu, na wa umeme. Majengo hayo yana ofisi 122, kutia ndani 80 za watafsiri; Jumba zuri la Ufalme; na jengo kubwa la kuchapia. Kuna majengo matatu ya makao yenye vyumba vizuri, dobi, chumba cha kulia, na jiko lenye vifaa vyote vinavyohitajika. Vifaa vingi vilivyotumiwa kujenga ofisi hiyo vilinunuliwa nchini humo, nayo ilijengwa kwa miaka miwili.
Kazi ya Ufalme ilianzishwa India mwaka wa 1905. Sasa vitabu hutafsiriwa na kuchapwa katika lugha 26 za India. Wakati wa kuwekwa wakfu kwa ofisi hiyo, wamishonari wengi waliokuwa wametumika India kwa miaka mingi walisimulia mambo mengi yaliyoonwa yenye kutia moyo. Hotuba ya kuweka wakfu ilitolewa na Stephen Lett wa Baraza Linaloongoza, na watu 2,933 waliisikiliza, wakiwemo wageni 150 kutoka nchi 25.
-
-
Matukio Muhimu Ya Mwaka Uliopita2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 29]
Ofisi ya Tawi iliyowekwa wakfu hivi karibuni huko Bangalore, India
-